Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mauaji wivu wa mapenzi yatisha wanaharakati “ni janga la kitaifa”
Habari Mchanganyiko

Mauaji wivu wa mapenzi yatisha wanaharakati “ni janga la kitaifa”

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi inayoshughulika na masuala ya ndoa, familia na malezi Tanzania (TaMCare), Dk. Enock Mlyuka
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imeombwa itangaze matukio ya ukatili katika ndoa hasa mauaji yanayosababishwa na wivu wa mapenzi, kuwa ni janga la kitaifa. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Wito huo umetolewa leo  Jumamosi, tarehe 7 Agosti 2021, katika warsha ya kuwajengea uwezo watetezi wa haki za binadamu katika kukabiliana na maafa na majanga, mkoani Dar es Salaam, iliyoandaliwa na Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC).

Akizungumza katika warsha hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi inayoshughulika na masuala ya ndoa, familia na malezi Tanzania (TaMCare), Dk. Enock Mlyuka, amesema matukio ya ukatili katika ndoa yanashamiri kwa kuwa hayazungumziwi kitaifa.

“Janga la ndoa na mahusiano hayazungumziwi, ikiwemo kuvunjika kwa ndoa na mauaji ya wivu wa mapenzi. Ili kukabiliana na hilo, inabidi ukatili wa kijinsia katika ndoa utangazwe ni janga la kitaifa,” amesema Dk. Mlyuka.

Dk. Mlyuka ameiomba Serikali na asasi za kiraia, ziendelee kutoa elimu kwa jamii juu ya athari za matukio hayo, ili yakomeshwe.

“Msisitizo wangu ni kwamba, elimu na mafunzo kwa vijana wa kike na wa kiume wanaotarajia kuoa na kuolewa,  wanahitaji kupewa uzito unaostahili. Na ndiyo kazi tunayofanya TaMCare kutoa ushauri nasaha ili kufanya kuwarejesha wanandoa katika hali ya kawaida,” amesema Dk. Mlyuka.

Mkurugenzi Msaidizi anayeshughulilia Maafa katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Charles Msangi, amesema ili matukio hayo yatokomezwe, Serikali itachukua  hatua za haraka  ikiwemo kutoa elimu kwa umma.

” Hili inabidi tuliseme ili watu wachukue hatua, kwa ajili ya kuokoa watoto wetu ambao wanathirika baada ya mfarakano au mauaji,” amesema Msangi.

Hivi karibuni kumekuwa na wimbi kubwa la mauaji ya wivu wa mapenzi. Ambapo Jeshi la Polisi Tanzania limesema katika kipindi cha Mei hadi Juni 2021,  kulikuwa na matukio ya mauaji ya wivu wa mapenzi 21.

1 Comment

  • Hii inatokana na kukiuka taratibu za Mwenyezi Mungu, kuwaweka mbele waganga wa ramli, kufanya matambiko ndio matokeo ya ndoa na mahusiano yote kulega na kuvunjika mapema mno na ushauri wa uongo wa wazazi na walezi.
    Tunatakiwa tangu tunazaliwa tuwe upande wa mungu tu, waislam waswali swala tano kila siku wafunge na kukamilisha maagizo ya mungu bila kukwepa hata siku moja kama ambavyo mungu ameagiza.
    wakristu nao waegamie upande wao wa kumuabudu mungu akama inavyotakiwa kula kunywa kuvaa na kufunga na kutubu, masuala ya tambiko na waganga wa kienyeji watabiri waawaache kabisa maana hayo ndio mamb ya mashetani na ndio yanayoua ndoa kila siku.
    kifupi ukiingiza mambo ya waganga wa kienyeji, watabiri, mashetani majini sijui nini yaani ukimuongeza mwingine zaidi ya mungu utapata matatizo makubwa sana katika ndoa yako hata ufanye nini maana unaweza kumjengea mwanamke wako nyumba tano na bado akakudharau na ukakuta humhitaji kabisa njia ni ya munguyeye ndie alietuumba na njia zake ndio zitakazo tufanya tuishi duniani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!