Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mashambulizi Afrika Kusini: Tanzania yasitisha safari zake 
Habari MchanganyikoKimataifa

Mashambulizi Afrika Kusini: Tanzania yasitisha safari zake 

Spread the love

SERIKALI imesitisha safari za Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) kwenda Afrika Kusini, kufuatia vurugu zinazoendelea nchini humo. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Raia wa taifa hilo, wamekuwa wakiwashambulia raia wageni wanaofanya shughuli mbalimbali nchini humo kwa madai, wanachukua kazi zao.

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 5 Septemba 2019 na Mhandisi Isack Kamwelwe, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Mhandisi Kamwelwe amesema, ATCL limesitisha safari zake kwenda nchini humo hadi pale Tanzania itakapopokea taarifa za maandishi kutoka kwa Serikali ya Afrika Kusini, kuhusu hali ya usalama.

” ATCL imesitisha safari zake za nchini Afrika ya Kusini kufautia vurugu zinazoendelea nchini humo, mpaka pale ambapo Serikali ya Tanzania itapokea taarifa za kimaandishi kutoka kwa Serikali ya Afrika Kusini,” amesema Mhandisi Kamwelwe.

Wakati Tanzania kupitia ATCL ikisitisha safari zake, raia wa Nigeria waishio nchini Afrika Kusini wamepewa usafiri wa bure na serikali yao warudi nchini mwao, ili kujiokoa na mashambulio dhidi ya raia wa taifa hilo.

Geoffrey Onyeama, Waziri wa Mambo ya Nje wa Nigeria akizungumza na wanahabari tarehe 4 Septemba 2019 nchini humo, amesema kwa Wanaigeria waliotayari kurejea nchini mwao, wawasiliane na Tume Kuu ya nchi hiyo iliyoko mjini Pretoria au ofisi ya balozi Mkuu wa nchi hiyo jijijni Johannesburg, kwa ajili ya utaratibu zaidi.

Hata hivyo, Onyeama amesema hakuna raia wa Nigeria aliyepoteza maisha katika fujo hizo, na kueleza kwamba mamlaka husika zitadai fidia kwa mali za raia wake zilizoharibiwa katika shambulio hilo.

Wakati Nigeria ikitangaza uamuzi huo, nchi kadhaa zimetoa tamko kuhusu fujo hizo, ikiwemo Botswana ambayo imewataka raia wake kutofika maeneo yenye fujo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!