Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo Mashabiki 10,000 kuiona Stars
Michezo

Mashabiki 10,000 kuiona Stars

Spread the love

 

 Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) limeruhusu mashabiki 10,000 kuingia uwanjani kwenye mchezo wa kufuzu fainali kombe la Dunia kesho kati ya timu ya Tanzania ‘Taifa Stars’ dhidi ya Benin. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mchezo huo wa kundi J, utapigwa kesho Alhamisi Oktoba 7, 2021 majiora ya saa 10 jioni katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es Salaam.

Akizungumza kuelekea mchezo huo Afisa Habari na Mawasiliano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania ‘TFF’ Clifford Ndimbo amesema kuwa Caf wameruhusu idadi ya mashabiki 10,000 kutazama mchezo huo.

“Tumepokea taarifa ya kuruhusiwa mashabiki 10,000 kushuhudia mchezo wa kesho na tayari tumeshaweka viingilio rafiki kuhakikisha watu wanajitokeza kwa wingi kuipa sapoti timu yao.” Alisema Ndimbo

Taifa Stars inaingia kwenye mchezo huo huku wakiwa vinara kwenye kundi J, wakiwa na pointi nne mara baada ya kucheza michezo miwili.

Akitaja Viingilio hivyo Afisa Habari huyo alisema kuwa kiingilio cha chini kitakuwa shilingi 3000 kwa kuwa kitakuwa rahisi kwa kila mtu.

“Viingilio vilivyowekwa ni 5000 kwa VIP B na C na shilingi 3000 kwa mzunguko, utaona kiingilio ambacho kila mmoja anaweza kukimudu na tujitokeze Uwanjani kesho”.

Mara baada ya mchezo Star itasafiri usiku kuelekea nchini Benin kwa ajili ya mchezo wa marudiano kundi J, utakaopigwa Oktoba 10, 2021

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!