Mchengelwa ameyasema hayo leo tarehe 24 Juni 2019 bungeni Jijini Dodoma katika kipindi cha maswali na majibu.
Amesema, tatizo la uhaba wa maji katika jimbo lake ni kubwa, hali inayopelekea wananchi kutembea umbali mrefu kutafuta huduma hiyo, huku wengine wakithubutu kuchota maji katika mto rufiji ambao una mamba wengi.
Kufuatia changamoto hiyo, Mchengelwa ameihoji serikali ina mpango gani wa kuiondoa changamoto hiyo.
“Tatizo la maji kwenye Wilaya ya Rufji ni kubwa sana, hali iliyopelekea nguvu kubwa ya vijana na kina mama kupotea wakijaribu kutembeea umbali mrefu na kudiriki kuchota maji mto rufiji. Na kupeleka wananchi wengi kuchukuliwa na mamba,” amesema Mchengelwa na kuongeza;
“Serikali ina mpango gani wa kuja kufanya tathimini ikizingatiwa kwamba Rufiji ni kanda maalum na pia tunatekeleza mradi wa kufua umeme wa stiegler’s Gorge, lini itakuja kufanya tathimini ya tatizo la maji . Wananchi wanatumia km 7 mpaka kumi kutafuta maji, lini serikali itachimba visima virefu ili kuwaondolea adha wananchi.”
Akijibu swali hilo, Jumaa Aweso, Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji amesema serikali inatambua changamoto hiyo na kwamba imefanya jitihada mbalimbali katika kukabiliana nayo ikiwemo kujenga visima virefu 13 katika jimbo hilo.
Aweso amesema baada ya ujenzi wa visima kukamilika, serikali itafanya usanifu kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mikubwa ya maji.
“Tunatambua maji ni uhai na ni moja ya changamoto kubwa, tumefanya jitihada kubwa ya kuchimba visima 13 pale vyenye thamani ya zaidi milioni 400. Tumeshachimba 10 , baada ya ukamilikishaji wa visima tutafanya usanifu katika kuhakikisha tunafanya miradi mikubwa ili wananchi wako wapate maji, “ amesema Aweso.
Leave a comment