Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Mahakama yampa onyo kali Wema
Michezo

Mahakama yampa onyo kali Wema

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam imerejesha dhamana ya Wema Sepetu, Msanii wa Filamu nchini huku ikimpa onyo la kutorejea kukiuka masharti ya dhamana. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Wema alifutiwa dhamana yake tarehe 11 Juni 2019 na Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama hiyo, Maira Kasonde baada ya kukiuka masharti yake.

Kwenye kesi hiyo, upande wa serikali unawakilishwa na Wakili Jenifer Masue, huku upande wa utetezi ukiwakilishwa na Albert Msando na Ruben Simwenzi.

Baada ya kukaa kwa wiki moja mahabusu, leo terehe 24 Juni 2019, mahakama hiyo imeamua kurejesha dhamana yake ambayo ilizuiwa kutokana na Wema kushindwa kuhudhuria kwenye kesi hiyo hapo awali.

Msanii huyo ambaye pia ni Miss Tanzania 2006, anakabiliwa na tuhumza za kuchapisha picha za uchi kwenye mtandao na kisha kusambaza.

“Mahakama inakuonya, pale haupo mahakamani kwasababu yoyote ile ijulishe mahakama, mshitakiwa anapokuwa nje kwa dhamana, anakuwa chini ya ulinzi wa mdhamini.

“Endapo akishindwa mdhamini, ataondolewa na mahakama itamfutia dhamana mshtakiwa…kwa sasa tunakupa onyo na dhamana yako itaendelea,” amesema Hakimu Kasonde. Kesi hiyo itatajwa tena tarehe 4 Julai mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Ujanja ni kubeti na Meridianbet

Spread the love  JUMAPILI ya leo imekaa kihela hela sana ndani ya...

error: Content is protected !!