Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mama Janeth Magufuli atoa misaada kwa wahitaji
Habari Mchanganyiko

Mama Janeth Magufuli atoa misaada kwa wahitaji

Spread the love

 

MAMA Janeth, Mjane wa aliyekuwa Rais wa wa Tanzania, John Pombe Magufuli amesema, ataendeleza utamaduni waliyojiwekea yeye na marehemu mume wake wa kutoa misaada kwa wenye uhitaji wakati wa sikukuu za kidini ili kugawana na wenzao kidogo walichojaaliwa nacho. Anaripoti Mwandishi Wetu, Geita … (endelea).

Mama Janeth ameyasema hayo leo Ijumaa, tarehe 18 Machi 2022, wakati akikabidhi misaada mbalimbali kwa kaya 100 zenye uhitaji, wafungwa, pamoja na watoto yatima katika hafla fupi iliyofanyika nyumbani kwake Chato mkoani Geita.

Amesema ameamua kutoa misaada hiyo katika kipindi hiki ambapo waumini wa dini ya Kikristo duniani kote wako katika mfungo wa Kwaresima wa siku 40 ikiwa ni ishara ya kushiriki mateso pamoja na Yesu Kristo, aliyejitoa sadaka kuteswa, kufa msalabani na baada ya siku tatu akafufuka ili kumkomboa mwanadamu.

“Kipindi cha Kwaresima ni cha kufunga na kufanya toba. kutafakari maisha yetu, tujikane nafsi zetu kwa kutenda matendo mema na kujizuia kutenda vitendo viovu ili kujisogeza karibu na Mwenyezi Mungu,” amesema.

“Katika kipindi hiki tunaaswa kusaidia wenye uhitaji na shida mbalimbali kwani (Mithali 19:17) Amhurumiaye masikini humkopesha Bwana; Naye atamlipa kwa tendo lake jema,” amesema Mama Janeth

Misaada hiyo ameitoa ikiwa ni siku moja baada ya kuadhimisha kumbukizi ya mwaka mmoja wa kifo cha Hayati Magufuli kilichotokea tarehe 17 Machi 2021, jijini Dar es Salaam na mwili wake kuzikwa nyumbani kwao Chato.

Kumbukizi hiyo ilifanyika jana na na iliyoongoza na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.

Misaada alioyotoa ni pamoja na mchele tani 3.2, Maharage tani 3.4, sabuni za miche za kufulia katoni 50 pamoja na sare za wanafunzi 500, ikiwa ni za wasichana jozi 250 na idadi hiyo hiyo ya jozi kwa wavulana.

Hafla hiyo ilihudhuriwa pia na Mkuu wa Wilaya ya Chato, Martha Mkupasi, Mbunge wa Chato, Dk. Medard Kalemani, Mkuu wa Gereza la Chato, Raphael Magesa, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Batholomew Manunga pamoja na viongozi wa dini, wadau wa maendeleo na wananchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!