Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Makonda: Chama kitafuata mkondo wake kuhusu Gekul
Habari za SiasaTangulizi

Makonda: Chama kitafuata mkondo wake kuhusu Gekul

Spread the love

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema taratibu zitafuata mkondo wake kupitia mamlaka za nidhamu kuhusu tuhuma za udhalilishaji zinazomkabili Mbunge wa Babati mjini, Pauline Gekul (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 27 Novemba 2023 jijini Dar es Salaam, Katibu wa NEC itikadi na Uenezi CCM, Paul Makonda amesema chama hicho kina kanuni na taratibu.

“Kuhusu mbunge wa babati mjini, chama chetu kina kanuni na taratibu… na sisi ngazi ya Taifa tunajua kuna mamlaka kuanzia ngazi ya tawi alilotokea, kuanzia wilaya hadi kwenda mkoa na itakapofikia Taifa tutatoa taarifa ya nini kimetokea lakini kanuni zipo na tuna timu ya mamlaka ya nidhamu na kama jambo litabainika basi taratibu zitafuata mkondon wake,” amesema Makonda.

Kauli hiyo ya CCM imekuja wakati mbunge huyo akidaiwa kutoa maelekezo kwa kundi la vijana kumdhalilisha kwa kumpiga na kumwingiza chupa sehemu ya haja kubwa na kumtishia kumpiga mfanyakazi wake risasi, Hashim Ally.

Tuhuma dhidi ya Gekul ambaye pia alikuwa Naibu Waziri wa Sheria na Katiba, zilianza kusambaa mitandaoni hivi karibuni na video yenye urefu wa takribani dakika 4: 03 zilimuonyesha kijana Ally akielezea unyama aliofanyiwa huku akiomba msaada.

Wakati tuhuma hizo zikizidi kushika kasi huku watetezi wa haki za binadamu wakijitokeza kulisemea sakata hilo, Rais Samia Suluhu Hassan alitengua uteuzi wa naibu waziri huyo.

Aidha, Kamanda wa polisi wa mkoa wa Manyara, Kamishna msaidizi George Katabazi naye amenukuliwa akiwataka wakazi wa mjini Babati kuwa watulivu wakati wao wakiendelea na uchunguzi wa tukio la kijana huyo.

“Tunawaomba watu watupe nafasi tufanye kazi yetu, hakuna mtu yetote aliye juu ya sheria hapa nchini, wasijali tunasimamia upatikanaji wa haki kwa mujibu wa sheria zilizopo,”amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!