Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Majangili yatelekeza porini nyara za serikali
Habari Mchanganyiko

Majangili yatelekeza porini nyara za serikali

Meno ya tembo
Spread the love

JESHI la Polisi mkoani Mbeya kwa kushirikiana  na askari wa TANAPA wamekamata pikipiki sita  zikiwa zimepakia nyara za serikali katika pori la hifadhi ya Taifa la Ruaha liliopo katika kijiji cha  Nyamlala  tarafa ya Rujewa wilayani Mbarali, anaandika Mwandishi Wetu.

Nyara zilizokamatwa ni pamoja na ngozi moja ya simba na vipande 15 vya meno ya tembo vikiwa vimepakiwa katika pikipiki hizo huku zikiwa zimetekelezwa na wahusika ambao walikimbia.

Tukio hilo limetokea baada ya kuwapo msako mkali wa  jeshi la polisi na askari wa TANAPA katika hifadhi hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Kamanda wa polisi Mkoani Mbeya , Mohammed Mpinga amesema baada ya pikipiki hizo kukamatwa wahusika walikimbia na kuzitekeleza katika pori hilo.

Kamanda Mpinga amesema kati ya pikipiki hizo, mbili zilikuwa hazina namba za usajili huku nyingine zikiwa ni  MC 386 BHW aina ya Kinglion, MC T.799 CTW aina ya T-Better, MC 755 ADJ, T.461 BZE.

Aidha, Mpinga amesema pikipiki hizo baada ya kukaguliwa zilikutwa na nyara za serikali ambazo ni ngozi moja ya Simba na vipande 15 vya meno ya Tembo.

“ Upelelezi na ufuatiliaji unaendelea ili kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hili ili waweze kuchukukuliwa hatua zinazostahili”amesema  Kamanda Mpinga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!