Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Majaliwa mashindano ya SHIMIWI yarejeshwe
Michezo

Majaliwa mashindano ya SHIMIWI yarejeshwe

Spread the love

 

WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa ameziagiza wizara zote zinazohusika na uratibu na uandaaji wa Michezo ya Wizara na Idara za Serikali Tanzania (SHIMIWI) wahakikishe wanakutana na kuweka mpango wa kurejesha michezo hiyo ili watumishi wa umma wapate fursa ya kushiriki na kujikinga na maradhi yasiyoambukiza. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Amesema michezo hiyo ya SHIMIWI ni muhimu kwa sababu ilikuwa inawakutanisha Watumishi wa Wizara za Serikali na Taasisi zake na ilisaidia sana kuboresha afya zao na kuongeza hamasa ya utendaji kazi hivyo kuongeza tija na ufanisi wa kazi.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo Jumapili, tarehe Agosti 15, 2021 wakati alipomuwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan wakati wa mbio za hisani za “CRDB Bank Marathon” zilizofanyika katika viwanja vya The Greens, Oysterbay Dar es Salaam.

Majaliwa amesema mashindano hayo ya SHIMIWI yaliwasaidia watumishi wa umma kupambana na magonjwa sugu yasiyoambukiza tofauti na sasa. “Nakumbuka mara ya mwisho michezo hii ilifanyika mwaka 2014.”

“…naelekeza Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jinsia, Wazee na Watoto na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ili kuweka mikakati ya pamoja ya kufufua michezo na ushiriki wa michezo kwa watumishi, wanafunzi na wananchi kwa ujumla,” amesema.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa

Kadhalika, Waziri Mkuu ameiagiza TAMISEMI ihakikisheni inasimamia kwa ukaribu ushiriki wa michezo kwa watumishi na wananchi, pia michezo kama vile jogging, marathon, mchakamchaka nayo inatakiwa ipewe kipaumbele hususan kwa wanafunzi.

“Natambua kuwa Katibu Tawala wa Mkoa (RAS) na Katibu Tawala wa Wilaya (DAS) ni wenyeviti wa Kamati za Michezo za Mikoa na Wilaya katika maeneo yao. Kwa hiyo, hakikisheni mnalisimamia jambo hilo.”

Majaliwa amesema Serikali kwa upande wake imeruhusu shughuli za michezo ziendelea kwa kutambua umuhimu wake katika kuimarisha afya za binadamu pamoja na kujikinga na ugonjwa wa UVIKO19. “Mazoezi kama ilivyo lishe ni muhimu sana kwenye kulinda mwili dhidi ya maradhi mbalimbali ikiwemo UVIKO19.”

Waziri Mkuu amesema kwa upande huo wa mazoezi, Shirika la Afya Duniani (WHO) linashauri watu wafanye mazoezi ya walau dakika 150 kwa wiki (yaani dk 30 kila siku kwa siku 5 za juma). “Haya ni mazoezi ya kiwango cha chini kama vile kutembea, kuendesha baiskeli.”

“Kwa msingi huo, binafsi ninafarijika sana kuona mwitikio huu mkubwa kutoka kwa Watanzania pamoja na wageni kwenye tukio hili adhimu. Kwa lugha nyingine, ushiriki wenu kwenye mbio hizi za CRDB Bank Marathon ni kielelezo tosha kuhusu utayari na utu mlionao katika kuchangia watoto wetu kupata huduma za upasuaji wa moyo.”

Amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango huo katika kuwapunguzia mzigo wazazi na walezi wa watoto hawa.

“Nyote mtakubaliana nami kuwa kuuguza si jambo la lelemama hasa unapouguza mtoto. Jambo la kuuguza mtoto husababisha wasiwasi na maumivu kwa wazazi na walezi hasa tunapokuwa tukishuhudia watoto wetu wakiugulia maumivu ya ugonjwa.”

“Nimefahamishwa kuwa ushiriki wenu kwenye mbio hizi, utawezesha upatikanaji wa fedha za kuanzisha Kituo cha Taarifa za Saratani (Cancer Information Centre) katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road. Kituo hiki kitakuwa kiungo muhimu kati ya wagonjwa wa saratani, wanaohudumia wagonjwa wa saratani na wale wenye wasiwasi juu ya saratani.

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela alisema hii ni mara ya pili kwa benki hiyo kuandaa mbio hizo, Agosti mwaka 2020 ambapo zaidi ya watu 4,000 walichangia watoto 100 kupata tiba ya upasuaji wa moyo katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete kwa gharama ya Sh.200 milioni.

Alisema lengo la mbio za mwaka huu ni kuendelea kushirikiana na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete na kuanzisha Kituo cha Taarifa za Saratani (Cancer Information Centre) katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road pamoja na kuimarisha afya zao kwa kufanya mazoezi huku wakijumuika na familia, rafiki na jamii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!