Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli awahoji wanaotaka akae madarakani miaka mitano
Habari za Siasa

Magufuli awahoji wanaotaka akae madarakani miaka mitano

Rais John Magufuli, mgomba Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CCM
Spread the love

MGOMBEA urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Magufuli amewahoji wananchi wanaotaka akae madarakani muhula mmoja tofauti na walivyokaa marais waliopita. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Rais wa awamu ya Kwanza, Mwalimu Julius Nyerere alikaa madarakani zaidi ya miaka 20 huku waliomfuata Dk. Ali Hassan Mwinyi (awamu ya pili), Benjamin Mkapa (awamu ya tatu) na Jakaya Kikwete (awamu ya nne) waliongoza miaka 10 kila mmoja ambayo ni sawa na mihula miwili.

Rais Magufuli aliyeingia madarakani tarehe 5 Novemba 2015 amesema, kwa nini watu hao wanataka wampunzishe ilihali amekaa madarakani miaka mitano.

Akizungumza na wananchi wa Jimbo la Chemba mkoani Dodoma leo Jumatatu tarehe 26 Oktoba 2020, amewaomba Watanzania wamchague tena akamilishe miaka yake 10.

“Nyerere alikaa miaka 20 na kitu, alitutafutia uhuru akang’atuka mwenyewe, akaja Mzee Mwinyi akakaa miaka 10 akaondoka, marehemu Mkapa kakaa miaka 10 akapumzika, akaja Kikwete amekaa miaka 10 akampumzika, mimi nimekaa miaka mitano mnataka mnipumzishe.”

Rais John Magufuli akizindua kitabu cha Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, wengine ni wastaafu, Jakaya Kikwete na Ali Hassan Mwinyi

“Mtanipa miaka mitano mingine nifikishe kumi kama wenzangu,” amewahoji wananchi hao ambao walimuahidi kumchagua.

Rais Magufuli amewaahidi wananchi wa Chemba na Watanzania kwa ujumla akichaguliwa kuwa Rais wa Tanzania ataongeza kasi ya utatuzi wa changamoto zao sambamba na kuwaletea maendeleo.

Aidha, amewasihi Watanzania kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa amani, ikiwa sambamba na kurudi nyumbani baada ya kupiga kura Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!