Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea aiandikia barua NEC, IGP Sirro
Habari za Siasa

Kubenea aiandikia barua NEC, IGP Sirro

Saed Kubenea, Mgombea Ubunge jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya ACT-Wazalendo
Spread the love

MGOMBEA Ubunge Kinondoni kupitia ACT-Wazalendo, Saed Kubenea ameiandikia barua Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), akiiomba imwondoe Msimamizi wa Uchaguzi Wilaya ya Kinondoni, Aaron Kagurumjuli. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Kubenea amedai Kagurumjuli anakiuka sheria na kanuni za uchaguzi, hali inayoweza kusababisha uchaguzi utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 kutokuwa huru na haki.

Hayo ameyasema leo Jumatatu leo tarehe 26 Oktoba 2020 wakati anazumgumza na wanaandishi wa habari Ofisi za Makao Makuu ya ACT-Wazalendo, Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Kubenea amesema, Kagurumjuli anaonesha waziwazi kumpendelea Mgombea Ubunge wa CCM katika jimbo hilo, Abbas Tarimba.

IGP Simon Sirro

Ameishauri NEC kufuatilia kwa ukaribu muenendo wa Kagurumjuli na matukio yanayoendelea katika mchakato wa uchaguzi kwenye jimbo hilo.

“Mimi binafsi, nimeaindikia barua Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuiomba ama imuengue kusimamia kazi hii ya kitume ama ifuatilie kwa karibu mienendo na matukio ya Kinodnoni ili uchaguzi uishe kwa usalama na amani ili anayeshinda uchaguzi ndio atangazwe mshindi,” amesema Kubenea.

Amesema, nakala ya barua hiyo ameiwasilisha kwa Inspekta Jenerali wa Polisi Tanzania (IGP), Simon Sirro na Mwenyekiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage.

Marehemu Akwilina Akwilin

“Na barua, nimeinakili kwa mwenyekiti NEC,  IGP Sirro ili imuondoe kwa kuwa ana viashiria vya U-CCM vilivyobobea na vinavyoweza kuhatarisha amani,” amesema Kubenea.

Kubenea amekumbushia kile kilichotokea katika uchaguzi mdogo wa Ubunge wa Kinondoni Februari mwaka 2018 ambapo Kagurumjuli alichelewa kuwapatia barua za utambulisho mawakala wa Chadema.

Amesema, hatua hiyo Chadema waliandamana kwenda ofisi za msimamizi wa uchaguzi huo (Kagurumjuli) ambapo ilitokea vurugu iliyosababisha kifo cha Mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwiline.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!