HATUA ya 16 ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya itaendelea hii leo kwa kupigwa michezo miwili, ambapo Real Madrid itakuwa ugenini kuvaana na PSG ya nchini Ufaransa. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Mchezo huo wa mtoano utapigwa majira ya saa 5 usiku kwenye dimba la Parc De Princes nchini Ufaransa.
Tukio la kuvutia kwenye mchezo huo ni kumshuhudia Sergio Ramos akishuka dimbani kwa mara ya kwanza dhidi ya timu yake ya zamani aliyoitumikia katika kipindi cha miaka 16 akiwa kama nahodha.
Mchezaji huyo aliondoka ndani ya Madrid kwenye dirisha kubwa la usajili, na kujiunga na matajiri hao wa jijini Paris kwa uhamisho huru.
Kabla ya mchezo huu wa leo Real Madrid na PSG wamekutana mara sita, kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa na Madrid wamefanikiwa kuondoka na ushindi kwenye michezo mitatu na kwenda sare mara mbili, huku PSG akiibuka na ushindi kwenye michezo mmoja tu.
Kwenye michezo hiyo, Real Madrid wamefanikiwa kupachika jumla ya mabao nane kwenye michezo yote sita, tofauti ya bao moja kwa PSG ambao wamefunga mabao saba.
Mchezo mwengine hii leo utapigwa kwenye dimba la Jose Alvalade nchini Ureno, ambapo Sporting Lisbon itashuka dimbani dhidi ya Manchester City na nchini England.
Leave a comment