KOCHA mpya wa Simba ya Tanzania, Pablo Franco amewasili nchini humo kuanza kibarua ya kuwanoa mabingwa hao watetezi wa ligi kuu na kombe la shirikisho. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam …(endelea).
Pablo ambaye ni raia wa Hispania, amewasili leo Jumatano, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Soma zaidi:-
Kocha huyo anakuja kuchukua mikoba ya Didier Gomes ambaye hivi karibuni, walikubaliana kuvunja mkataba.
Ni baada ya Simba kutolewa kwenye michuano ya Klabu Bingwa Afrika na sasa inashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Leave a comment