MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Musoma Vijijini (1980-1985), Herman Kirigini, unatarajiwa kuzikwa leo Jumamosi, kijijini kwao Muryaza, Wilaya ya Butiama. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mara … (endelea).
Kirigini alifarikini dunia tarehe 23 Mei 2023, baada ya kuanguka ghafla akitoka chumbani kwake katika nyumba yake iliyoko Musoma Mjini, mkoani Mara.
Jana Ijumaa tarehe 26 Mei 2025, mwili wa kirigini ulitolewa heshima za mwisho nyumbani kwake Musoma Mjini, kisha ulisafirishwa kuelekea Butiama kwa ajili ya mazishi.
Kufuatia msiba huo, Mbunge wa Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo, ametoa salamu za rambirambi kwa familia, ndugu jamaa na marafiki, huku akichangia mahitaji mbalimbali kufanikisha mazishi.
Miongoni mwa michango hiyo ni, mchele kilo 100, maharage kilo 30, ssukari kilo 25, ngano kilo 25 na mafuta lita 20.
Mbali ya kuwa mbunge, Kirigini aliwahi kuwa Waziri wa Kilimo na Mifugo.
Leave a comment