Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko IGP Sirro apangua makamanda wa mikoa
Habari Mchanganyiko

IGP Sirro apangua makamanda wa mikoa

Spread the love

MKUU wa jeshi la polisi nchini (IGP), Simon Sirro, ametangaza mabadiliko ya makamanda wa mikoa katika jeshi lake kwa kuhamisha baadhi huku na kupeleka kule. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Miongoni mwa waliohamishwa, ni pamoja na aliyekuwa Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza, Naibu Kamishena, Ahmed Msangi ambaye ameletwa makao makuu ya upelelezi jijini Dar es Salaam.

Msangi amefanywa kuwa mkuu wa kitengo cha makosa dhidi ya binadamu.

Taarifa ya mabadiliko hayo imetolewa leo tarehe 15 Agosti 2018 na msemaji wa jeshi hilo, Kamishena msaidizi wa polisi, Barnabas Mwakalukwa.

“Uhamisho huo ni mabadiliko ya kawaida yanayotokea ndani ya Jeshi la Polisi katika kuongeza ufanisi wa utendaji kazi,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Sehemu ya taarifa hiyo pia imeeleza kuwa  nafasi ya DCP Msangi, imechukuliwa na aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Jonathan Shana.

Naye aliyekuwa mkuu wa operesheni Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Wankyo Nyigesa, amechukua nafasi ya Shana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!