ALIYEKUWA Katibu wa Chama cha Riadha Tanznia (RT), Wilhelim Gidabuday amejiuzuru nafasi yake kwenye shirikisho hilo baada ya kushaulina na kukubaliana na kamati tendaji kwa maslahi mapana ya shirikisho hilo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).
Kidabuday amechukua uamuzi huo jana baada ya kufanya kikao cha muda mrefu na maamuzi yake kukubaliwa na kamati tendaji ya shirikisho huku akiahidi kuendeleza ushirikiano na viongozi waliobaki.
“Sababu ya mimi kujiuzuru mbele ya kamati ya utendaji kwa ajili ya maslahi mapana ya shirikisho la riadha, siyo kwamba niliowaacha ni wabaya ila ile njia nilioitaka mimi haijaungwa mkono na wengi,” alisema Kidabuday.
Aidha Kidabuday aliongezea kuwa ameondoka kwa nia njema na amewashukuru wajumbe wote na kuahidi kuwaunga mkono katika utendaji wao wa kazi.
Kamati tendaji ya shirikisho hilo imemteua Ombeni Zavara kukaimu nafasi hiyo hadi hapo uongozi utakapo mtangaza katibu mkuu atakayekuja kuchukua nafasi hiyo iliyoachwa wazi.
Ikumbukwe mwaka 2012, Gidabuday alijipatia umaarufu mara baada ya kuahidi kuchoma vyeti vyake moto kama timu ya taifa ya riadha ingefanikiwa kurudi na medali katika mashindano ya Olimpiki yaliyofanyika jijini London, England.
Baada ya miaka miwili, Kidabuday alifanikiwa kuchaguliwa kuwa mtendaji mkuu wa riadha nchini, mara baada ya kumshinda Gidamis Shahanga kwenye uchaguzi wa chama hicho na kuunda safu ya uongozi akiwa na Anthony Mtaka ambaye alikuwa Raisi wa shirikisho hilo.
Leave a comment