Tuesday , 30 May 2023
Home Kitengo Michezo Gidabuday aweka wazi sababu ya ya kujiuzuru RT
Michezo

Gidabuday aweka wazi sababu ya ya kujiuzuru RT

Spread the love

ALIYEKUWA Katibu wa Chama cha Riadha Tanznia (RT), Wilhelim Gidabuday amejiuzuru nafasi yake kwenye shirikisho hilo baada ya kushaulina na kukubaliana na kamati tendaji kwa maslahi mapana ya shirikisho hilo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Kidabuday amechukua uamuzi huo jana baada ya kufanya kikao cha muda mrefu na maamuzi yake kukubaliwa na kamati tendaji ya shirikisho huku akiahidi kuendeleza ushirikiano na viongozi waliobaki.

“Sababu ya mimi kujiuzuru mbele ya kamati ya utendaji kwa ajili ya maslahi mapana ya shirikisho la riadha, siyo kwamba niliowaacha ni wabaya ila ile njia nilioitaka mimi haijaungwa mkono na wengi,” alisema Kidabuday.

Aidha Kidabuday aliongezea kuwa ameondoka kwa nia njema na amewashukuru wajumbe wote na kuahidi kuwaunga mkono katika utendaji wao wa kazi.

Kamati tendaji ya shirikisho hilo imemteua Ombeni Zavara kukaimu nafasi hiyo hadi hapo uongozi utakapo mtangaza katibu mkuu atakayekuja kuchukua nafasi hiyo iliyoachwa wazi.

Ikumbukwe mwaka 2012, Gidabuday alijipatia umaarufu mara baada ya kuahidi kuchoma vyeti vyake moto kama timu ya taifa ya riadha ingefanikiwa kurudi na medali katika mashindano ya Olimpiki yaliyofanyika jijini London, England.

Baada ya miaka miwili, Kidabuday alifanikiwa kuchaguliwa kuwa mtendaji mkuu wa riadha nchini, mara baada ya kumshinda Gidamis Shahanga kwenye uchaguzi wa chama hicho na kuunda safu ya uongozi akiwa na Anthony Mtaka ambaye alikuwa Raisi wa shirikisho hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

NBC Dodoma Marathon yazinduliwa, wakiambiaji 6,000 kushiriki

Spread the loveBENKI ya NBC imetangaza kufanyika kwa mbio kubwa za NBC...

Michezo

Rais Samia anunua tiketi 5000 Yanga vs USM Alger

Spread the loveRAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu...

Michezo

Mwenyekiti UVCCM anogesha nusu fainali Kimwanga CUP, Hawa Abdul Rede CUP kwa kishindo

Spread the loveHEKAHEKA za michuano ya kuwania kuingia fainali ya michuano ya...

Michezo

Yanga SC. yatwaa ubingwa wa pili mfululizo

Spread the love  KLABU ya Yanga SC imeweka rekodi ya kutwaa ubingwa...

error: Content is protected !!