Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo FIFA: Ya Sepp Blatter yamkuta Infantino
Michezo

FIFA: Ya Sepp Blatter yamkuta Infantino

Spread the love

TUHUMA za rushwa ndani ya Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), limechepua tena na sasa Gianni Infantino, rais wa shirika hilo amefunguliwa jalada la uchunguzi. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Infantino anatuhumiwa kuingilia uchunguzi uliofanywa na FIFA dhidi ya Sepp Blatter mwaka 2015, aliyekuwa rais wa shirika hilo kwa kutoa taarifa za uongo na kwa maslahi binafsi. Infantino aliapishwa kuwa rais wa FIFA tarehe 26 Februari 2016.

Kwa mujibu wa mwendesha mashtaka wa Uswisi Stefan Keller, wiki iliyopita, Infantino alifunguliwa jalada la uchunguzi kuhusu kuhusika kwake, ni baada ya kuonekana kuwepo kwa viashiria vya Infantino kufanya vigisu wakati wa uchunguzi wa Blatter.

Hata hivyo, Infantino amepuuza madai hayo ambayo sasa yanaripotiwa kwa kiwango kikubwa na vyombo vya habari vya Uswisi na Ujerumani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!