Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Fedha tozo miamala ya simu zatimiza ndoto wananchi Madaba
Habari Mchanganyiko

Fedha tozo miamala ya simu zatimiza ndoto wananchi Madaba

Spread the love

WANANCHI wa Materereka katika Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, mkoani Ruvuma wamesema ujenzi wa kituo cha afya kilichojengwa kwa fedha za tozo za miamala umekuwa kama ndoto kwao kwa sababu hawakutarajia kusogezewa karibu huduma za matibabu. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Wananchi walieleza hayo juzi mbele ya Mkurugenzi Mtendaji wa halmshauri ya Madaba, Sajidu Mohamed aliyefanya ziara ya kukagua mwenendo wa ujenzi wa kituo hicho kilichogharimu Sh milioni 250.

Kituo hicho kimejengwa katika eneo ambalo litasaidia asilimia kubwa ya wananchi kupata huduma za matibabu kwa urahisi bila kulazimika kwenda maeneo mengine ya jirani.

Mmoja wa wananchi hao, Constatine Mlelwa amesema wanaona kama ndoto kwa namna walivyokuwa wakihangaika kupata huduma za matibabu, wakilazimika kutumia gharama kubwa kwenda hospitali ya wilaya ya Madaba au mkoani.

“Kwa niaba ya wananchi wa Matetereka tunamshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi wake wa kutujengea kituo cha afya hapa. Kituo hiki kitatumika na wananchi wa vijiji vya Maweso, Matetereka na Mwande kwa sababu hata upasuaji utafanyika hapa,” alisema Mlelwa.

Naye Deograsius Mponda anayeishi Matetereka akiwa na watoto saba, amemshukuru Rais Samia kwa kuwaona kwa jicho la huruma kwa kuwasogezea huduma za matibabu kwa ngazi ya kituo cha afya akisema wamekuwa wakipata adha ya kutembea umbali mrefu kutafuta matibabu.

“Nina watoto saba lakini natamani nizae mtoto mwingine katika kituo hiki cha jirani maana kipo karibu na makazi yangu. Mungu ambariki Rais Samia kwa moyo wake wa upendo wa kuwajali wananchi mbalimbali hasa wa vijijini.

 

Thobias Ngelangela-‘Babu Matetereka’

Kwa upande wake, Rogatha Matei mkazi wa kijiji cha Mwande amesema huduma za afya wanapata katika zahanati ya Matetereka lakini wakihitaji matibabu makubwa wanalazimika kutembea umbali wa kilomita zaidi ya 20 hadi Madaba.

“Umbali wake ukipanda pikipiki Sh 1,000 hadi halmashauri, tulikuwa changamoto kubwa hasa wajawazito ambapo kama huna fedha huwezi kufika Madaba. Lakini kituo hiki kikikamilika kitakuwa mkombozi mkubwa kwa wakazi wa Matetereka.

Akizungumzia ujenzi huo, Mkurugenzi Mtendaji, Mohamed amesema ujenzi huo unakaribia kukamilika na kituo hicho kikianza kutoa huduma kitakuwa msaada mkubwa kwa wakazi wa Materereka ambao kwa nyakati tofauti walilazimika kufuata huduma ya matibabu huko Madaba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!