Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Ebola yaibuka tena Congo
Habari MchanganyikoTangulizi

Ebola yaibuka tena Congo

Spread the love

MLIPUKO wa Virusi vya Ebola, umeibuka tena Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC). Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Taarifa ya mlipuko huo, imetolewa na wizara ya afya nchini humo, ambapo inaeleza mtu mmoja kutoka Mji wa Biena karibu na mji wa Butembo Jimbo la Kivu Kaskazini, amefariki dunia kutokana na virusi hivyo.

Taarifa ya wizara hiyo inasema, inapeleka timu ya wataalamu katika eneo hilo lenye mlipuko.

Jana Jumapili tarehe 7 Februari 2021, Umoja wa Mataifa (UN) , ulisema hadi saa watu 70 wamebainika walikuwa karibu na wagonjwa wa Ebola katika eneo hilo.

“Zaidi ya watu 70 wametambuliwa kuwa walikuwa na makaribiano na mgonjwa huyo aliyefariki dunia na kazi ya kutakasa maeneo aliyokuwa ametembelea inaendelea,” inaeleza taarifa ya UN.

Taarifa ya UN inasema, sampuli zilizochukuliwa kutoka kwa wagonjwa wawili ambao mmoja wake amefariki dunia, zimepelekwa maabara kuu ya Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa nchini DRC (INRB), ili kutambua aina ya virusi hivyo.

Naye Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Kanda ya Afrika, Dk. Matshidiso Moeti, amesema, shirika hilo linasaidiana na mamlaka husika kufanya uchunguzi, ili kubaini kutokomeza mlipuko wa Ebola.

Kwa mujibu wa mitandao ya kimataifa, mlipuko huo ni wa 12 kutokea nchini humo, ambapo mlipuko wa mwisho ulitokea Septemba 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!