Saturday , 25 March 2023
Habari MchanganyikoTangulizi

Ebola yaibuka tena Congo

Spread the love

MLIPUKO wa Virusi vya Ebola, umeibuka tena Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC). Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Taarifa ya mlipuko huo, imetolewa na wizara ya afya nchini humo, ambapo inaeleza mtu mmoja kutoka Mji wa Biena karibu na mji wa Butembo Jimbo la Kivu Kaskazini, amefariki dunia kutokana na virusi hivyo.

Taarifa ya wizara hiyo inasema, inapeleka timu ya wataalamu katika eneo hilo lenye mlipuko.

Jana Jumapili tarehe 7 Februari 2021, Umoja wa Mataifa (UN) , ulisema hadi saa watu 70 wamebainika walikuwa karibu na wagonjwa wa Ebola katika eneo hilo.

“Zaidi ya watu 70 wametambuliwa kuwa walikuwa na makaribiano na mgonjwa huyo aliyefariki dunia na kazi ya kutakasa maeneo aliyokuwa ametembelea inaendelea,” inaeleza taarifa ya UN.

Taarifa ya UN inasema, sampuli zilizochukuliwa kutoka kwa wagonjwa wawili ambao mmoja wake amefariki dunia, zimepelekwa maabara kuu ya Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa nchini DRC (INRB), ili kutambua aina ya virusi hivyo.

Naye Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Kanda ya Afrika, Dk. Matshidiso Moeti, amesema, shirika hilo linasaidiana na mamlaka husika kufanya uchunguzi, ili kubaini kutokomeza mlipuko wa Ebola.

Kwa mujibu wa mitandao ya kimataifa, mlipuko huo ni wa 12 kutokea nchini humo, ambapo mlipuko wa mwisho ulitokea Septemba 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mchina wa SGR aburuzwa kortini kwa kumjeruhi Mtanzania, TRC waja juu

Spread the love  RAIA wa China, Zheng Yuan Feng, amefikishwa mahakamani kwa...

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

error: Content is protected !!