Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Michezo Dube, Sure Boy kuikosa Simba
Michezo

Dube, Sure Boy kuikosa Simba

Spread the love

MSHAMBULIAJI wa klabu ya Azam FC, Prince Dube pamoja na kiungo wa klabu hiyo, Salum Abubakar ‘Sure Boy’ wataokusa mchezo dhidi ya Simba mara baada ya kupata majeruhi. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea)

Mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, utapigwa kesho kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi majira ya saa 1 usiku.

Akithibitisha kukosekana kwa wachezaji hao, kocha msaidizi wa klabu hiyo, Vivier Bahati amesema kuwa wachezaji hao pamoja na Aggrey Morris watakosekana kutokana na sababu za kiafya.

“Katika mchezo wa kesho, tutamkosa mshambuliaji wetu Prince Dube anayesumbuliwa na majeruhi, pia kiungo wetu Sure Boy ambaye amepata homa pamoja na nahodha, Agrrey Morris,” alisema kocha huyo.

Azam FC wanaingia kwenye mchezo huo, huku wakiwa na kumbukumbu ya kupoteza kwa bao 1-0, kwenye mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup)

Katika mchezo wa mzunguko wa kwanza kwenye ligi, timu hizo zilifungana mabao 2-2.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!