Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Michezo Mashabiki elfu 10, kutazama fainali Simba na Yanga Kigoma 
MichezoTangulizi

Mashabiki elfu 10, kutazama fainali Simba na Yanga Kigoma 

Spread the love

 

KUELEKEA mchezo wa fainali wa kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup), idadi ya mashabiki watakaoruhusiwa kutazama mchezo huo ni elfu 10 tu, na tiketi za mchezo huo zitaanza kuuzwa kuanzia Julai 19 Mwaka huu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mchezo huo safari hii utapigwa mkoani Kigoma juali 25 mwaka huu, majira ya saa 9:30 jioni.

Akizungumza jana usiku kupitia kipindi cha michezo cha Wasafi Redio, mkurugenzi wa mashindano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Salum Madadi alisema kuwa “Kwa Uwanja huu hatutoruhusu kuingiza watu zaidi ya 10,000.” 

Raia Mwema lilipomtafuta kutaka ufafanuzi zaidi juu ya idadi hiyo ya mashabiki na ukubwa wa mchezo huo, Madadi alisema kuwa hawezi kulizungumza hilo kwa sasa mpaka watakapo kaa kikao na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa.

“Tiketi zitaanza kuuzwa tarehe 19 mwezi huu, ila idadi ya kuwa zitauzwa ngapi kwa sasa bado ila tutatangaza, baada ya kikao cha kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa.” Alisema Madadi

Aidha katika upande mwengine wa maandalizi ya mchezo huo, Madadi alisema kuwa mpaka sasa wameshapiga hatua kubwa, hasa kwenye eneo la Uwanja.

Kikosi cha Simba

“Tupo vizuri na tumepiga hatua kubwa hasa kwenye eneo la kuchezea ‘Pitch’ na miundombinu mingine ya Uwanja na kila kitu kinaenda sawa.” Alinena Mkurugenzi huyo wa mashindano.

Mchezo huo utakuwa wan ne kuwakutanisha wababe hao wawili katika msimu mmoja, katika michezo mitatu iliyopita Yanga ilifanikiwa kushinda miwili ukiwemo wa Ligi Kuu Tanzania Bara na fainali ya kombe la Mapinduzi sambamba na kwenda sare mechi moja.

Simba inakwenda kucheza mchezo huo huku wakiwa mabingwa wapya wa Ligi Kuu, na walifuzu fainali hiyo kwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0, kwenye mchezo wa nufu fainali dhidi ya Azam FC.

Mshambuliaji wa Yanga, Yacouba Sogne akishangilia bao lake

Kwa upande wa Yanga wanaenda kwenye mchezo huo, huku wakiwa na rekodi ya kupata matokeo kwenye mchezo uliopita dhidi ya Simba, kwa bao 1-0, na walitinga fainali hiyo mara baada ya kuifunga Biashara United kwa bao 1-0.

1 Comment

  • Hapa kuna kuvaa barakoa na kuepuka msongamano? Tumewaahidi wafadhili kuwa tutatekeleza maagizo ya wataalamu kuhusu Covid halafu tunapuuza?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia ampandisha cheo RPC wa Dar

Spread the loveMKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Camillus Wambura, amesema...

Habari za SiasaTangulizi

Wanachama 384 CUF watimkia Chadema, Mbowe awapokea, Kambaya ndani…

Spread the loveJUMLA ya wanachama 384 wanachama wa Chama cha Wananchi CUF...

error: Content is protected !!