Tuesday , 21 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Doreen apokea watoto 3 wa Mrema wa nje ya ndoa
Habari MchanganyikoTangulizi

Doreen apokea watoto 3 wa Mrema wa nje ya ndoa

Spread the love

 

MJANE wa Marehemu Agustino Mrema amesema hadi sasa ameshapokea watoto watatu wa nje ya ndoa wa mume wake ambao walikuwa hawajapokewa na kwamba kitendo hicho ni kutimiza husia wake kwake kabla ya kufariki. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro … (endelea).

Doreen ameyasema hayo leo Jumanne tarehe 30, Agosti, 2022, wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Moshi ikiwa ni siku chache tangu kuzikwa kwa Mrema.

“Kabla hajafariki Baba (Mrema) alinihusia niwapokee na kuwalea kwa upendo na umoja watoto wake wote waliopo na hata wale watakaoibuka baadae na kusema ni wanae, akanielekeza nisiogope, niwapokee, nimuombee radhi kwenu, niwakumbatie na kuwalea kama ambavyo angefanya yeye,” amesema Doreen na kuongeza;

“Mpaka sasa nimeshawapokea watoto watatu (3) ambao walikuwa bado hawajapokelewa na nilishaambiwa hivyo na Mzee Mrema siku mbili kabla ya kifo chake.”

Aidha amesema muda sahihi ukifika nitasema ukweli wote ikwemo masuala ambayo yameibuliwa na vyombo vya habari.

“Muda ukifika nitasema, siogopi na Mzee Mrema alisema nisiogope hata wakati akiwa hayupo,” amesisitiza.

Inadaiwa kumekuwepo na mgogoro mkubwa baina ya ndugu wa Mrema na Doreen ambao ulianza hata kabla ya maziko yake ambapo ndugu hao waliitoa matairi gari ambayo ilikuwa itumike na ndugu wa mwanamke huyo kwenda msibani Moshi.

Inaelezwa kuwa gari hiyo aina ya Toyota Harrier ilitolewa matairi yote manne ikiwa nyumbani kwa Mrema Salasala jijini Dar es Salaam ikiwa tayari imeshapakiwa mizigo ya ndugu wa Doreen, kitendo ambacho kilionesha ndugu hao kumtenga.

Taarifa zaidi kutoka ndani ya familia hiyo zinaeleza kuwa matairi hayo yalitolewa na mkwe wa Mrema ambaye inadaiwa alieleza kufanya hivyo kwasababu hawamtambui Doreen kama sehemu ya familia hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Watumishi 25,039, taasisi 65 wahamia Dodoma

Spread the loveSerikali imesema hadi sasa, jumla ya watumishi 25,039 kutoka Serikali...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yapata idhini kuwa wakala wa madalali wa DSE

Spread the loveBenki ya NMB imepata idhini kutoka Benki Kuu ya Tanzania...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Waziri aipongeza NBS kwa mafanikio

Spread the loveNaibu Waziri wa Fedha, Hamad Chande amepongeza Ofisi ya Taifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Balozi Nchimbi aonya maofisa utumishi kuacha uonevu

Spread the loveKatibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel...

error: Content is protected !!