DAKTARI Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), amesema “ni kweli vyuma vimekazi” akaongeza “kwa wale wapiga dili.” Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Kiongozi huyo wa chama tawala, yumo jijini Dar es Salaama akiendelea na ziara yake ya kichama katika Jimbo la Ubunge linaloongozwa na Saed Kubenea (Chadema) ikiwa ni siku yake ya pili.
Akizungumza leo tarehe 28 Agosti 2019 katika Shule ya Msingi Ubungo Kisiwani Dk. Bashiru amesema, ni wakati wa kufanya kazi na sio kukaa ‘vijiweni’ kwamba wale wasiokuwa na kazi maalumu wataendelea kulalamika.
“Vijana waachane na tabia ya uvivu kwani uvivu ni adui wa maendeleo… muda wa kupata dezo umepita,” amesema Dk. Bashiru na kuongeza; “vijana muache kukatishana tamaa.”
Amesema, ikiwa vyuma vimekazwa kwa sababu ya kujenga shule, kuokoa vifo vya kina mama, kulina uhuru na amani bado vyuma hivyo viendelee kukaza mpaka Watanzania tushike adabu.
Dk. Bashiru anaendelea na ziara yake kwenye jimbo hilo, ambapo baadaye ataanza ziara katika jimbo la Kibamba linaloongozwa na John Mnyika (Chadema).
Leave a comment