Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Diwani aililia serikali ya Rais Magufuli
Habari Mchanganyiko

Diwani aililia serikali ya Rais Magufuli

Prof. Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu
Spread the love

WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imeombwa kuangalia uwezekano wa kuipa usajili shule ya sekondari ya Matuli iliyopo wilayani Morogoro vijijini ili ianze kutumika,  anaandika Christina Haule.

Hatua hiyo itawasidia wanafunzi  wa eneo hilo wanaotembea kilimita 21  kwenda shule ya sekondari ya kata ya  Ngerengerea.

Ombi hilo limetolewa leo na na Diwani wa Kata ya Matuli Tarafa ya Ngerengere katika Halmashauri ya Morogoro vijijini, Lukas Lemomo kwenye mkutano wa hadhara na wananchi wake kuzungumzia maendeleo ya elimu kwenye kata hiyo.

Diwani huyo amesema kuwa licha ya  majengo ya shule hiyo kukamilika kwa ajili lakini imeshindwa kaunza kuchukua wanafunzi kutokana na kutokamilisha usajili.

Amesema kukosekana kwa usajili wa shule hiyo kumefanya wanafunzi kulazimika kusoma shule iliyopo kata nyingine ambayo ipo umbali mrefu.

“Tayari  madarasa mawili ya kidato cha kwanza na cha pili tumeshayajenga kwa kushirikisha nguvu za wananchi kwa na katika kipindi cha miaka miwili tutakuwa tayari tumemalizia madarasa mengine mawili wakati watoto wanaendelea kusoma, Waziri Ndalichako tunaomba liangalie hili ” amesema

Aidha,  amewaomba wananchi kutochoka kuendelea kuchangia na kujitolea katika kuhakikisha kata hiyo inapata shule ya kata ya sekondari na kwamba fedha zote zinazochangwa zipo salama katika akaunti ya kata na zitatumika kuendeleza ujenzi kama ilivyopangwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!