Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa DC Katambi awachimba mkwara wapinzani kuhoji ulinzi wa Rais
Habari za Siasa

DC Katambi awachimba mkwara wapinzani kuhoji ulinzi wa Rais

Spread the love

PATROBAS Katambi, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma amesema, watu wanaohoji ulinzi wa rais hawana nia njema. Anaripoti Hamis Mguta… (endelea).

Na kwamba, watu hao kama wangehoji ulinzi alionao Rais John Magufuli wakiwa Dodoma, angewakamata na kuwatia ndani.

Akizungumza na MwanaHALISI Online ofisini kwake jijini humo amesema, viongozi wa serikali hawapo tayari kumwangusha rais kwa lolote.

“Hatupo tayari kumuangusha Rais Magufuli kwasababu amefanya mambo makubwa. Eti unakuta kuna wapumbavu nasikia wanauliza kwanini rais ana ulinzi mkubwa? ni upuuzi,” amesema.

Katambi ameeleza kuwa, kwa sasa hakuna tajiri anayeweza kuvunja sheria kwasababu ni tajiri na kwamba, hiyo inatokana na rais kuwachukulia hatua mapema.

Bila kumtaja jina Katambi amesema, “huku ni kufilisika kwa hoja, tunawaona wengine walikuwa na watu wanaitwa Red bridged, vijana wengi halafu wanawashindisha na njaa, hawawapi hata chakula, mbona wao hatuwaulizi? Na mimi nilikuwa huko na ninafahamu vijana wale walikuwa wanafanya kazi kwa moyo sana.

“Kiongozi alikuwa na walinzi zaidi ya saba na alikuwa anawashindisha njaa, akishamaliza mambo yake utasikia ‘Komaa Kamanda” halafu anapanda V8 anaondoka, nyie mnatembea kwa miguu,” amesema.

Katambi alijiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) akitokea chama kikuu cha upinzani, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Jumanne ya tarehe 21 Novemba 2017.

Akiwa Chadema, alikuwa Mwenyekiti wa Barza la Vijana la chama hicho (Bavicha).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!