Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo Chama arejea, Manula, Lwanga ‘Out’ dhidi ya Mbeya City
MichezoTangulizi

Chama arejea, Manula, Lwanga ‘Out’ dhidi ya Mbeya City

Spread the love

Mara baada ya kukosekana Uwanjani kwa wiki tatu, kiungo wa klabu ya Simba, Clatous Chama amerejea Uwanjani, huku mlinda mlango wa klabu hiyo Aishi Manula pamoja na Thadeo Lwanga wataukosa mchezo wa leo dhidi ya Mbeya City kwa kutumikia adhabu ya kadi tatu za njano. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Chama amerejea mara baada ya kufiwa na mke wake Mercy Manuka tarehe 29 Mei 2021, Kitwe nchini Zambia.

Mchezo huh, utapigwa hii leo majira ya saa 1 usiku, kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam.

Akithitisha taarifa za wachezaji hao, kocha msaidizi wa klabu ya Simba Seleman Matola amesema kuwa kiungo huyo ameshawasili kambini na kujiunga na wenzake, mara baada ya timu hiyo kurejea kutoka Mwanza.

“Kikosi kiliingia kambini jana baada ya kurejea kutoka Mwanza kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wetu wa kesho na tunafurahi kiungo Clatous Chama amewasili na amejiunga na wenzake.” Alisema Matola

Aidha Matola pia alithibitisha kukosekana kwa wachezaji wawili kwenye mchezo wa leo kutokana na kuwa na kadi tatu za njano, huku mmoja akiwa anaumwa.

Thadeo Lwanga, kiungo wa Simba

“Manula na Taddeo wao watakosekana kwenye mchezo wa kesho sababu wana kadi tatu za njano wakati Ibrahim Ajibu ni mgonjwa anasumbuliwa na malaria lakini wachezaji wengine wote wako fiti tayari kwa mechi,” amesema Matola.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

error: Content is protected !!