Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge kuanza na miswada 3 ya uchaguzi
Habari za SiasaTangulizi

Bunge kuanza na miswada 3 ya uchaguzi

Bunge
Spread the love

Mkutano wa 14 wa Bunge la 12 uliopangwa kufanyika kwa muda wa wiki tatu kuanzia kesho tarehe 30 Januari hadi tarehe 16 Februari 2024 unatarajiwa kuanza kujadili miswada mitatu iliyowasilishwa kwa mara ya kwanza bungeni Novemba mwaka jana. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Miswada hiyo ambayo imeibua mjadala pamoja na kupingwa na wadau mbalimbali ikiwamo vyama vya siasa, imetajwa kuwa na uzito wa kipekee kiasi cha kuongezewa muda wa wiki moja tofauti na utaratibu wa kawaida wa bunge kukaa wiki mbili.

Taarifa iliyotolewa leo Jumatatu na Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Kimataifa, Ofisi ya Bunge imesema miswada ambayo imepangwa kujadiliwa katika mkutano huo ni Muswada wa Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa Mwaka 2023 na Muswada wa Sheria ya Tume ya Uchaguzi wa Mwaka 2023.

Miswada mingine ni Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria za Vyama vya Siasa wa Mwaka 2023 na muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali (Na.5) wa Mwaka 2023.

Vilevile katika mkutano huu wa Bunge Kamati za Kudumu za Bunge zitawasilisha taarifa za shughuli zlzotekelezwa na Kamati kwa mwaka 2023.

Aidha, taarifa hiyo imesema wastani wa maswali 250 ya kawaida na maswali 24 ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu yanatarajwa kuulizwa na wabunge.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!