Friday , 17 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge kuanza kesho, fedha za Corona kutikisa
Habari za Siasa

Bunge kuanza kesho, fedha za Corona kutikisa

Spread the love

 

MKUTANO wa Tano wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, unatarajiwa kuanza kesho tarehe 2 Novemba, mwaka 2021 huku matumizi ya fedha za mkopo nafuu wa Shirika la Fedha Duniani (IMF) kwa ajili ya kukabiliana na athari za UVIKO-19 yakitarajiwa kujadiliwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Ofisi Bunge leo tarehe 1 Novemba, 2021 imebainisha kuwa shughuli kubwa kesho itakayofanyika katika Ukumbi wa Msekwa ni Bunge kupokea maelezo kuhusu maeneo ya vipaumbele ya matumizi kuhusu fedha hizo.

Aidha, kwa mujibu wa ratiba hiyo, siku ya Jumatano tarehe 3 Novemba, 2021 Kamati ya Mipango itawasilisha Mapendekezo ya Mpango wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023.

Mapendekezo ya mpango huo yatajadiliwa kwa muda wa siku tano kabla ya Bunge kupokea maelezo kuhusu miradi ya nishati ya umeme ya kimkakati na hatua zilizofikiwa katika utekelezaji wake.

Bunge hilo litaahirishwa tarehe 12 Novemba mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yatoa kauli wanaolala nje Hospitali ya Muhimbili

Spread the loveSERIKALI imesema inajipanga kushirikiana na sekta binafsi kujenga majengo yatakayosaidia...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara yaomba bajeti ya Sh. 67.9 bilioni, wamachinga watengewa bilioni 10

Spread the loveBAJETI ya Wizara ya maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yahamasisha uanzishaji vituo vya kulea watoto wachanga

Spread the loveSERIKALI imewahimiza wananchi kujenga vituo vya kulelea watoto wadogo na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

error: Content is protected !!