Tuesday , 21 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Barrick yang’ara maonesho ya OSHA- 2023, yatwaa tuzo 6, mshindi wa jumla
Habari Mchanganyiko

Barrick yang’ara maonesho ya OSHA- 2023, yatwaa tuzo 6, mshindi wa jumla

Spread the love

KAMPUNI ya Barrick Tanzania imenyakua tuzo sita katika kilele cha maadhimisho ya siku ya afya na usalama mahali pa kazi yanayofanyika katika Viwanja vya Tumbaku mjini Morogoro. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro… (endelea).


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Prof. Joyce Ndalichako akikabidhi tuzo ya OSHA mshindi wa jumla wa maonesho hayo Mkufunzi wa Usalama mahali pa kazi wa Barrick Bulyanhulu, Azaely Kitenge (katikati) ni Mwenyekiti wa Bodi ya OSHA, Dkt. Adelhelm Meru.

Katika maadhimisho hayo ambayo yanaratibiwa na Wakala wa Afya na Usalama Mahali pa kazi (OSHA), Mgodi wa Dhahabu wa Barrick Bulyanhulu, umeshinda tuzo kubwa ya mshindi wa juu wa jumla katika Tuzo ya Afya na Usalama (OHS) 2023.

Mbali na ushindi huo mkubwa, Bulyanhulu pia ilinyakua tuzo ya uandaaji ripoti bora ya tathmini ya hatari katika uchimbaji madini na mshindi bora wa tuzo ya usalama na afya (OHS) katika sekta ya madini.

Wafanyakazi wa Barrick wakifurahia tuzo mbalimbali ambazo kampuni imenyakua katika maonesho ya OSHA 2023

Kwa upande wake, Mgodi wa Barrick North Mara, ilishinda tuzo za juu katika: Kujali zaidi wafanyakazi wenye mahitaji maalum na utekelezaji sera bora ya usalama mahali pa kazi (OHS). Pia ilikuwa mshindi wa pili kwa washindi wa jumla wa sekta ya Madini.

Mwaka huu mgodi wa Buzwagi pia ulishiriki maonesho hayo na kunyakua tuzo ya utekelezaji mpango kazi bora wa usalama na afya mahali pa kazi.

Akizungumza katima kilele cha maadhimisho hayo Aprili 28, 2023 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu, Profesa Joyce Lazaro Ndalichako ambaye alikuwa mgeni rasmi alisisitiza waajiri kuzingatia sheria ya afya na usalama mahali pa kazi.

Aliwataka waajiri wote nchini kuchukua hatua ya kuhakikisha wanalinda usalama na afya za wafanyakazi wao kama yalivyomatakwa ya Sheria ya Afya na Usalama Mahali pa Kazi Namba 5 ya mwaka 2003.

Kampuni hiyo ya Barrick Tanzania imeshinda tuzo za 2023 kutokana na mafanikio ya 2022 ya kampuni ambapo ilishinda tuzo za jumla ikiwemo tuzo ya mshiriki wa maonyesho na tuzo ya kuzingatia kanuni za usalama.

Kampuni ina mpango maalum kwa ajili ya usalama wa wafanyakazi wake na wakandarasi, kuhakikisha kwamba kila mtu anarudi nyumbani akiwa na afya njema na salama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Geita, Mwanza waongoza kwa mbwa

Spread the loveNaibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Alexander Mnyeti amesema taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Watumishi 25,039, taasisi 65 wahamia Dodoma

Spread the loveSerikali imesema hadi sasa, jumla ya watumishi 25,039 kutoka Serikali...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yapata idhini kuwa wakala wa madalali wa DSE

Spread the loveBenki ya NMB imepata idhini kutoka Benki Kuu ya Tanzania...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Waziri aipongeza NBS kwa mafanikio

Spread the loveNaibu Waziri wa Fedha, Hamad Chande amepongeza Ofisi ya Taifa...

error: Content is protected !!