Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Askofu Ruwa’ichi kuongoza vijana 30,000 kuliombea Taifa
Habari MchanganyikoTangulizi

Askofu Ruwa’ichi kuongoza vijana 30,000 kuliombea Taifa

Spread the love

VIJANA zaidi ya 30,000 wanatarajia kukutana tarehe 17 Disemba, 2022 kwa ajili ya kuliombea taifa wakiongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Yuda Thadei Ruwa’ichi.

Askofu Thadei anatarajiwa kuongoza Ibada ya misa  ya  vijana hao katika mkesha wa kuliombea Taifa  utakaofanyika uwanja wa  Uhuru jijini Dar es salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Akizungumzia mkesha huo, Katibu wa maandalizi  wa mkesha huo, Ronaldo  Chota alisema  mkesha huo uliopewa jina la ‘Usiku wa sifa’, utafanyika usiku huo Jumamosi ambapo vijana watautumia katika  kuliombea Taifa.

Chota aliongeza kuwa wanafanya hivyo kama ambavyo viongozi wa nchi  wamekuwa wakihimiza watu kuliombea Taifa  ambapo  vijana wa  vyuo zaidi ya 51 vikitarajiwa kushiriki.

Aliongeza kuwa sio mara ya kwanza kuwa na mkesha  kwa ajili ya vijana kwani hata mwaka 2020 ulifanyika ambapo vijana 15,000 walihudhuria lakini kwa mwaka huu idadi hiyo itaongezeka na kufika hadi 30,000.

Hata hivyo, Mratibu huyo alieleza kuwa kwa vijana watakaofika katika mkutano huo pia watapata mafundisho yatakayowawezesha kupata hofu ya Mungu na kupata malezi bora ambayo yatakuja kuwasaidia kuwa viongozi bora wa kulitumikia taifa lao.

“Ni ukweli usiopingika kwa sasa kumekuwepo na changamoto nyingi  zinazowakumba vijana ikiwemo mmomonyoko wa maadili unaopelekea  kujiingiza katika vitendo viovu ikiwemo  uasherati, kutoa mimba na mambo mengine hivyo mkesha huu utatumika katika kuyatafakari haya  na kuona  namna ya kuepukana nayo,” alisema Chota.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Walei Jimbo la Dar es Salaam, Padri Vitalisi Kasembo, aliwaomba wazazi kuwaruhusu vijana wao kuhudhuria mkesha huo utakaowasiadia kuwajenga kiimani. 

Naye Mratibu wa  Karismatiki Katoliki Jimbo Kuu la  Dar es Salaam, Ludovic Kawishe, alisema usiku huo utasindikizwa na kwaya ya  Mtakatifu Makuburi na Lord’s Grace Team na Mwalimu Arbogast Kanuti ndiye  atakayehudumu.

Mkesha huo unatarajiwa kuanza saa tatu usiku mpaka saa 11 alfajiri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!