Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Asilimia 96 ya Watanzania wamefikiwa na mawasiliano ya simu
Habari Mchanganyiko

Asilimia 96 ya Watanzania wamefikiwa na mawasiliano ya simu

Spread the love

MTENDAJI Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Justina Mashiba, amesema asilimia ya 96 ya Watanzania wamefikiwa na huduma ya mawasiliano ya simu. Anaripoti Jonas Mushi…(endelea).

Mashiba amebainisha hayo leo Jumatatu tarehe 13 Februari 2023 wakati akielezea utekelezaji wa majukumu ya taasisi hiyo katika kuhahakikisha huduma nzuri ya mawasilino nchini.

Amesema kabla ya kuanzishwa kwa taasisi hiyo mwaka 2009 ni asilimia 45 tu ya Watanzania walikuwa wamefikiwa na huduma ya mawasiliano ya simu  kutokana na uwekezaji mwingi wa miundombinu kufanyika mjini.

Amesema idadi hiyo ya watu wanapata huduma za mawasilino ya simu kwa viwango tofauti ambapo asilimia 96 ni 2G na asilimia 72 kwa 3G na asilimia 55 wanapata 4G.

Kwa upande wa eneo la kijografia Mashiba amesema tayari asilimia 69 ya eneo la Tanzania limefikiwa na mawasiliano ya simu.

“Kijiografia hatujafanya vizuri sana na hii ni kutokana na maeneo mengi kuwa wazi na mengine kuwa ni hifadhi,” amesema Mashiba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!