Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT wazalendo wampa tano Samia kufufua mchakato Katiba mpya
Habari za Siasa

ACT wazalendo wampa tano Samia kufufua mchakato Katiba mpya

Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo, Ado Shaibu
Spread the love

CHAMA cha ACT Wazalendo kimeunga mkono na kuikaribisha kwa mikono miwili hatua ya Rais Samia Suluhu Hassan kumuagiza Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kuitisha kikao maalum cha Baraza la Vyama vya Siasa nchini kwa ajili ya kutathmini utekelezaji wa mapendekezo ya Kikosi Kazi cha kuratibu maoni ya wadau kuhusu demokrasia ya vyama vingi nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana tarehe 7 Mei 2023 na Katibu Mkuu wa chama hicho, Ado Shaibu,  imekuwa ni rai ya chama hicho kuhitaji ratiba ya utekelezaji wa mapendekezo ya kikosi kazi.

Amesema wanatarajia kikao hicho kitapatiwa ratiba hiyo ambayo itahakikisha kuna Sheria Mpya ya Uchaguzi na Sheria Mpya ya Vyama vya Siasa kabla ya mwisho wa mwaka huu.

“Vilevile kuhakikisha kwamba mabadiliko ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba yanafanyika ili kuanza mchakato wa Katiba Mpya kwa kuundwa kwa Timu ya Wataalam (Committee of Experts) kana ilivyopendekezwa na kikosi kazi.

“Ni mategemeo ya Chama chetu kuwa Baraza la Vyama vya Siasa itakuwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano wa Kitaifa ili kujadili mambo yaliyokwamisha mchakato wa Katiba wa 2014 na kupata mwafaka kwayo ili mchakato wa sasa usikwame,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!