Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT Wazalendo wajipanga kupaza sauti kuhusu tozo
Habari za Siasa

ACT Wazalendo wajipanga kupaza sauti kuhusu tozo

Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma wa ACT-Wazalendo, Janeth Rithe
Spread the love

 

HALMASHAURI Kuu ya Chama cha ACT-Wazalendo, imeiagiza Kamati ya Wasemaji ya Kisekta ya chama hicho kupaza sauti kuhusu changamoto ya kukithiri kwa tozo za Serikali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Hayo yamebainishwa leo Jumatatu, tarehe 5 Septemba 2022 na Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma wa ACT-Wazalendo, Janeth Rithe, akitoa maazimio ya kikao cha halmashauri hiyo kilichofanyika jana Jumapili, jijini Dar es Salaam.

Rithe amesema, mbali na kamati hiyo kupewa jukumu la kupaza sauti kuhusu tozo za Serikali, imetakiwa kujikita katika masuala ya uvunjifu wa haki za binadamu katika magereza na mageuzi katika Jeshi la Polisi, changamoto za bima ya afya na umuhimu wa hifadhi ya jamii.

“Halmashauri Kuu imeipongeza Kamati ya Wasemaji wa Kisekta kwa kazi kubwa inayoifanya ya kuwasemea Watanzania. Aidha, Halmashauri Kuu imeagiza Kamati ya Wasemaji wa Kisekta kupaza sauti juu ya maeneo mahsusi ya kukithiri kwa tozo za Serikali, uvunjifu wa haki za binadamu magerezani, changamoto za bima ya afya na umuhimu wa hifadhi ya jamii na mageuzi katika Jeshi la Polisi,” amesema Rithe.

Katika hatua nyingine, Rithe amesema Halmashauri kuu hiyo imepitisha azimio la kuundwa kwa kitengo cha kusimamia uwajibikaji wa Serikali ya Zanzibar.

“Halmashauri Kuu imepitisha Azimio la kuundwa kwa Kitengo cha Chama cha Kusimamia Uwajibikaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.Kitengo hicho kitakuwa na majukumu ya kufuatilia kwa karibu uwajibikaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kutoa sera mbadala,” amesema Rithe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!