MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim Lipumba, amekiwakilisha kituo hicho katika mkutano maalum wa kuvishawishi vyama vya siasa nchini Burundi, kujiunga katika baraza la siasa nchini humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma wa Chama cha Wananchi (CUF), Mhandisi Mohamed Ngulangwa, mkutano huo umefanyika leo Jumamosi, nchini Burundi.
Prof. Lipumba ambaye pia ni Mwenyekiti wa CUF Taifa, ameshiriki mkutano huo ili kuvishawishi vyama vya siasa ambavyo havijajiunga katika Baraza la Vyama vya Siasa Burundi, kujiunga.
Taarifa hiyo imesema baraza hilo lilianzishwa 2009 lakini hadi sasa vipo baadhi ya vyama havijajiunga.
Leave a comment