Sunday , 19 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Serikali yafafanua kuondolewa dawa 178 kitita cha NHIF
AfyaTangulizi

Serikali yafafanua kuondolewa dawa 178 kitita cha NHIF

Spread the love

SERIKALI imesema imeondoa dawa 178 katika kitita cha Mfuko wa Taifa wa Bima (NHIF), ili kupisha dawa bora zaidi zinazoendana na wakati wa sasa kwa magonjwa yote yanayowakumba watanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Ufafanuzi huo umekuja siku chache baada ya kuibuka vute ni kuvute kuhusu matumizi ya kitita hicho kilichohuishwa tarehe 18 Disemba mwaka jana na kupingwa na baadhi ya wamiliki wa hospitali binafsi.

Akitoa ufafanuzi leo Jumamosi Mkurugenzi wa Huduma za Dawa na Mfamasia Mkuu wa Serikali Daudi Msasi amesema baadhi ya dawa hizo zimeondolewa katika muongozo huo wa matibabu ili kuepuka uandishi wa dawa zenye muunganiko yaani Fixed Dose Combonation kwa kuwa nyingi zinakuwa zimebeba majina ya kibiashara.

Amesisitiza kuwa mwongozo huo umezingatia upatikanaji wa dawa zote muhimu kwa magonjwa yote nchini na kwa ngazi zote kuanzia Zahanati hadi Hospitali ya Taifa.

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu

Baadhi ya dawa zilizoondolewa ni zile zinazotibu magonjwa ya presha na sukari na wenye matatizo ya moyo.

Dawa za malaria kadhaa aina ya Artemether za vidonge, sindano na dripu pia zimeondolewa kwenye kitita hicho pamoja na dawa ya vidonge ya chloroquine inayotibu wenye selimundu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Afya

Kambi ya matibabu ya kibingwa Ruangwa yaacha vilio, DC atoa ombi JAI

Spread the loveMKUU wa Wilaya ya Ruangwa, Hassan Ngoma amefunga rasmi kambi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

Habari za SiasaTangulizi

Haya hapa majina walioteuliwa kugombea nafasi mbalimbali CHADEMA

Spread the loveCHAGUZI wa kanda za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)...

error: Content is protected !!