Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wabunge wataka magari ya mawaziri yatumie gesi kubana matumizi
Habari za Siasa

Wabunge wataka magari ya mawaziri yatumie gesi kubana matumizi

Spread the love

SERIKALI imetakiwa kuhakikisha magari ya viongozi wa umma wakiwemo mawaziri, yanabadilishwa mfumo wa matumizi ya mafuta kwenda gesi ili kubana matumizi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Wito huo umetolewa leo tarehe 15 Machi 2024 na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, ilipotembelea vituo vya kujazia gesi vilivyopo jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, David Mathayo, amesema gharama za gesi ni nafuu ikilinganishwa na mafuta ya dizeli na petroli, hivyo serikali inapaswa kuhakikisha magari ya viongozi yakayonunuliwa yanakuwa na mifumo ya moja kwa moja ya matumizi ya nishati hiyo.

“Kama mlivyosikia gharama ya gesi iko chini ukilinganisha kama mafuta ya kwaida ya dizeli na petrol na unakwenda umbali mrefu. Tunapenda kuwashauri TPDC na serikali kuwe na vituo vya kutosha. Tunashauri serikali na wauza magari wauze ambayo tayari yameshatengenezwa kw amfumo wa kutumia gesi hata magari ya serikali yanayoingia baadae yajipange yawe na mifumo ya gesi,” amesema Mathayo.

Katika hatua nyingine, Mathayo ameitaka Serikali kupunguza kodi katika vifaa vya kuweka mifumo ya gesi katika magari ili kupunguza gharama kwa lengo la kuvutiwa wananchi wengi kutumia gesi kwa gharama nafuu.

Pia, Mathayo ameishauri Serikali kuongeza idadi ya vituo vya kujaza gesi katika magari na karakana za kubadilisha mifumo.

Akijibu mapendekezo hayo, Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amesema Serikali itashirikiana na sekta binafsi kuhakikisha yanatekelezwa kikamilifu.

Amesema Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) imeandaa mkakati wa kuongeza vituo vya kujazia gesi kutoka idadi ya vitano iliyopo sasa hadi kufikia 15.

Akijibu mapendekezo hayo, Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amesema Serikali itashirikiana na sekta binafsi kuhakikisha yanatekelezwa kikamilifu.

Amesema Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) imeandaa mkakati wa kuongeza vituo vya kujazia gesi kutoka idadi ya vitano iliyopo sasa hadi kufikia 15.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

error: Content is protected !!