Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko 25 wafariki dunia katika ajali Arusha
Habari MchanganyikoTangulizi

25 wafariki dunia katika ajali Arusha

Spread the love

Watu 25 wamefariki dunia papo hapo mkoani Arusha katika ajali ya barabarani iliyohusisha magari matatu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha SACP Justine Masejo, kati ya watu hao watatu ni wa familia moja ya Abdulrazak Mohamed maarufu ‘Chucha’ wa Ngaramtoni.

Akizungumzia na waandishi wa habari Kamanda Masejo amesema ajali hiyo imetokea leo tarene 24 Februari majira ya saa 11 jioni baada ya lori lililokuwa likitokea Namanga kuelekea Arusha kuyagonga magari matatu.

Bila kutaja jina la dereva aliyekuwa akiendesha lori hilo, Kamanda Masejo amesema taarifa za awali zinaonyesha Lori  lilipoteza uelekeo hali iliyopelekea kuyagonga magari hayo.

Amesema majeruhi wa ajali hiyo wapo katika hali mbaya na wanaendelea na matibabu.

 Hata hivyo, amewaomba wananchi ambao ndugu zao walikuwa wakisafiri kupitia barabara hiyo kufika katika hospitali ya Mkoa wa Arusha Mount Meru kwa ajili ya utambuzi wa marehemu pamoja na majeruhi ambao wanatibiwa hapo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara yaomba bajeti ya Sh. 67.9 bilioni, wamachinga watengewa bilioni 10

Spread the loveBAJETI ya Wizara ya maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na...

Habari MchanganyikoTangulizi

Migogoro ya ndoa yaongezeka, Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveMIGOGORO ya ndoa na familia imeongezeka kwa asilimia 8.3  kutoka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yahamasisha uanzishaji vituo vya kulea watoto wachanga

Spread the loveSERIKALI imewahimiza wananchi kujenga vituo vya kulelea watoto wadogo na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

error: Content is protected !!