Monday , 20 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya DC Mpanda aagiza maji ya visima yapimwe kudhibiti kipindupindu
Afya

DC Mpanda aagiza maji ya visima yapimwe kudhibiti kipindupindu

Spread the love

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Jamila Yusuf ameziagiza mamlaka za afya na maji kushirikiana ili kuainisha idadi ya visima vilivyopo ndani ya wilaya hiyo na kuvipima kubaini maji ya visima hivyo yana usalama kiasi gani kwa matumizi ya binadamu. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Mkuu huyo wa wilaya ametoa maagizo hayo leo Ijumaa  katika kikao kazi maalum cha kuweka mikakati ya kukabiliana na magonjwa ya mlipuko hususani kipindupindu.

Amesema kila kaya inatakiwa kuzingatia suala la usafi wa mazingira, ikiwemo kunawa maji tiririka sanjari na kuwataka watumishi kuanzia ngazi ya serikali ya mtaa kuweka nguvu kazi katika kutunza mazingira, hiyo ikiwa ni njia mojawapo ya kukabiliana na magonjwa ya mlipuko.

Amewataka maofisa afya kufanya ukaguzi katika maeneo ya kutolea huduma ya chakula, stendi za mabasi na maeneo mengine yanayohusisha mkusanyiko wa watu, ikiwemo maeneo ya mabucha ili kuhakikisha udhibiti unaimarishwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Afya

Kambi ya matibabu ya kibingwa Ruangwa yaacha vilio, DC atoa ombi JAI

Spread the loveMKUU wa Wilaya ya Ruangwa, Hassan Ngoma amefunga rasmi kambi...

AfyaHabari za Siasa

Serikali yatoa kauli wanaolala nje Hospitali ya Muhimbili

Spread the loveSERIKALI imesema inajipanga kushirikiana na sekta binafsi kujenga majengo yatakayosaidia...

Afya

Mbunge ataka huduma Ultrasound itolewe bure kwa wajawazito

Spread the loveMBUNGE wa Viti Maalum, Esther Malleko, ameitaka Serikali kutoa bure...

Afya

Vituo 13 vyasitishiwa mkataba madai kutaka kupiga bilioni 4 za NHIF

Spread the loveVITUO vya kutoa huduma za afya 13, vimesitishiwa mikataba ya...

error: Content is protected !!