Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mawakili 10 TLS kumtetea mjane aliyehukumiwa miaka 22 kwa kuuza nyama ya swala
Habari Mchanganyiko

Mawakili 10 TLS kumtetea mjane aliyehukumiwa miaka 22 kwa kuuza nyama ya swala

Spread the love

CHAMA cha Mawakili wa Tanganyika (TLS) Kanda ya Iringa kimewataja mawakili 10 waliopangwa katika maandalizi na usikilizwaji wa rufaa ya hukumu ya kesi ya uhujumu uchumi namba 28 ya mwaka 2022 inayomuhusu mjane Maria Emirio Ngoda aliyehukumiwa miaka 22 kwa kosa la kukutwa na vipande 12 vya nyama ya swala. Anaripoti Mwandishi Wetun …(endelea).

Hukumu hiyo ilitolewa katika Mahakama ya Mkoa wa Iringa tarehe 3 Novemba 2023 na Hakimu Mkazi Mkuu Mkoa wa Iringa, Said Mkasiwa aliyedai kuridhishwa pasipo shaka kuwa mjane huyo mwenye watoto wanne alikutwa na ndoo iliyokuwa na nyama hiyo yenye thamani ya Sh 900,000.

Akitoa taarifa ya mchakato wa rufaa hiyo ikiwa ni siku moja baada ya TLS kanda hiyo kutangaza kumsaidia mjane huyo kufanya utetezi huo bure, Mwenyekiti wa TLS kanda ya Iringa, Wakili Moses Ambindwile alisema;

“TLS kwa kupitia mawakili hao tayari imepeleka Mahakama Kuu Kanda ya Iringa taarifa ya kukata rufaa na sasa tunasubiri kumbukumbu namba ya mfumo ili taratibu zingine ziendelee.

Mbali na yeye Wakili Ambindwile aliwataja mawakili wengine watakaosimama kumtetea mjane huyo ambaye rufaa ni sehemu ya haki yake kuwa ni pamoja na Dk Rwezaula Kaijage, Frank Ngafumika, Barnabas Nyalusi, Jane Massey, Samson Rutebuka, Joshua Chusi, Innocent Kibadu na Cosmas Kishamawe.

Tangu uhukumu hiyo dhidi ya mjane huyo itolewe na kuripotiwa katika vyombo mbalimbali vya habari ikiwemo mitandao ya kijamii kumejitokeza mijadala na hisia tofauti kuhusu maamuzi hayo ya Mahakama.

Baada ya TLS kujitokeza kumsaidia mjane huyo, jana imeripotiwa katika vyombo mbalimbali vya habari kuhusu nia ya Kamati ya Utekelezaji ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kumsaidia mjane huyo kukata rufaa.

Taarifa hiyo iliyotolewa na Mwenyekiti wa UWT Taifa, Mary Chatanda imeonesha kwamba “Pamoja na kwamba maamuzi ya mahakama ni maamuzi ya mahakama” UWT inajitolea kumsaidia mjane huyo katika rufaa yake kwa kuhakikisha anapata uwakilishi wa mawakili wa kutosha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari Mchanganyiko

Wananchi washauriwa kuongeza uelewa wa kujikinga na majanga

Spread the love WITO umetolewa kwa wananchi kuongeza uelewa na utayari kabla...

error: Content is protected !!