Friday , 17 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Msikimbilie kufanya kazi mijini – Ridhiwani Kikwete
Habari za Siasa

Msikimbilie kufanya kazi mijini – Ridhiwani Kikwete

Naibu waziri, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete,
Spread the love

 

NAIBU waziri, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, amewataka watumishi wa umma, kutokimbia kufanya kazi pembezoni mwa nchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Pwani … (endelea).

Akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Chalinze, leo Jumapili, Ridhiwani alisema, “hakuna sababu ya watumishi kuchagua mahali pakufanyia kazi.”

Aliwataka watumishi wa umma, kuendelea kuwahudumia wananchi wote sawa na hakuna sababu ya kuchagua na kuweka madaraja katika utoaji wa huduma.

Alisema, “…kutochagua vituo vya kazi, kunalenga sio tu kuwasaidia baadhi, lakini kunatengeneza madaraja katika utumishi wa umma.”

Akatumia mkutano huo kuwakumbusha watumishi umuhimu wa kufanya kazi kuzingatia misingi ya kazi ikiwemo kujitambua na kutambua tunaowahudumia.

Akaongeza: “Popote utakapopelekwa kuna hadhi ya mtumishi kuweza kufanya kazi. Nawaomba wazazi kuacha kupiga simu kuwaombea watoto wenu vibali vya kuhamishwa vituo ili wapelekwe mijini.”

Katika kikao hicho, Ridhiwani aliwapongeza watumishi wa halmashauri hiyo kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

ACT-Wazalendo yasusia uchaguzi wa ubunge Zanzibar

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo, kimegoma kushiriki uchaguzi mdogo wa Ubunge Jimbo...

error: Content is protected !!