Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko SUKITA yataka kamati za kutokomeza ukatili zianzishwe nchi nzima
Habari Mchanganyiko

SUKITA yataka kamati za kutokomeza ukatili zianzishwe nchi nzima

Spread the love

SERIKALI imetakiwa kuhakikisha kamati za Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya wanawake na watoto (MTAKUWWA), ngazi ya kata, zinaundwa nchi nzima ili kulinda haki za wananchi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Wito huo umetolewa leo tarehe 27 Julai 2023 katika mjadala kuhusu ujenzi na nguvu za pamoja juu ya kupambana na ukatili wa kijinsia na hamasa ya uundwaji kamati za MTAKUWWA, ulioandaliwa na Shirika la Usawa wa Kijinsia Tanzania (SUKITA) na kufanyika jijini Dar es Salaam.

Kaimu Mkurugenzi wa SUKITA, Msafiri Mwajuma Mariam amesema kamati hizo zikiundwa zitasaidia kupata mwarobaini wa matatizo ya ukatili wa kijinsia.

“Tunahamasisha uundwaji wa kamati za MTAKUWWA, kwani kama shirika tunaamini kama kamati hizi zikifanya kazi ipasavyo haya ya ukatili wa kijinsia yatakwisha kabisa,” amesema Msafiri.

Akisoma risala ya shirika hilo mbele ya mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo, Hilda Malosha, Mwanachama wa SUKITA, Cecilia Kimaro, ameiomba Serikali iendelee kutoa vibali kwa asasi za kiraia kwa ajili ya kutoa elimu kwa umma juu ya namna ya kutokomeza vitendo hivyo.

Afisa Miradi wa SUKITA, Jamaica Adam, amesema shirika lake limeandaa mjadala huo kwa ajili ya wadau kupata nafasi ya kubadilishana uzoefu wa namna ya kukabiliana na vitendo hivyo.

Akijibu risala ya SUKITA, Malosha amesema halmashauri hiyo itaendelea kutoa vibali kwa asasi za kiraia ili ziendelee kufanya kazi yake ya kutokomeza vitendo vya ukatili kwa ajili ya kuisaidia serikali.

“Elimu ni muhimu, kokote unapokuwa unawajibika kutoa elimu juu ya ukatili wa kijinsia ujue unapata swawabu kwa Mungu. Tutafurahi zaidi kama mtakuja kutoa elimu shuleni kote na tunaahidi kama halmashauri tuko pamoja na nyie,” amesema Malosha.

Naye Polisi Kata Makuburi, ASP Omary Fundi, ameishauri jamii iangalie kwa kina tatizo la ukatili wa kijinsia kwa kuwa ili liishe inatakiwa nguvu ya pamoja.


“Ukatili wa kijinsia ni mada pan asana, kwa hiyo ni jambo ambalo linahitaji tuliangalie kwa kina tuone namna gani tutapata suluhu,” amesema ASP Fundi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

error: Content is protected !!