Friday , 17 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia: Tusikubali mtu, kikundi kutugawa
Habari za Siasa

Rais Samia: Tusikubali mtu, kikundi kutugawa

Spread the love

Rais Samia Suluhu Hassan leo Jumanne ametoa wito kwa Watanzania kuwaenzi mashujaa kwa kudumisha amani, umoja, mshikamano na utulivu wa nchi na kufanya kazi kwa bidii kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu.

 

“Kamwe tusikubali mtu au kikundi cha watu kutugawa kwa kisingizio chochote kile, Tanzania ni moja na kamwe haitagawanyika,” amesema Rais Samia.

Xxxx

 

Rais Samia: Tusikubali mtu, kikundi kutugawa

 

RAIS Samia Suluhu Hassan amewataka ametoa wito kwa Watanzania kuwaenzi mashujaa kwa kudumisha amani, umoja, mshikamano na utulivu wa nchi na kufanya kazi kwa bidii kwa ajili ya maendeleo ya Taifa. Anaripoti Maryam Mudhihir…(endeleea).

Pia amewataka wananchi kutokubali watu au kikundi cha watu kuwagawa kwa kisingizio chochote.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 25 Julai 2023, katika maadhimisho ya siku ya kumbukumbu ya mashujaa ambayo yamefanyika kwa mara ya kwanza katika mji wa serikali Mtumba Jijini Dodoma.

“Kamwe tusikubali mtu yoyote au kikundi cha watu kutugawa kwa kisingizio chochote, Tanzania ni moja na kamwe haitagawanyika,” amesema Rais.

Pia ameiagiza ofisi ya waziri mkuu kusimamia ujenzi wa mnara mpya wa mashujaa wenye urefu wa mita 1,010 ambao utaweka rekodi ya kuwa mnara mrefu Afrika.

Aidha, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Uratibu na Bunge), Jenista Mhagama amempongeza rais kwa ujenzi huo wa mnara utakaokua kivutio na kuongeza kipato cha nchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

ACT-Wazalendo yasusia uchaguzi wa ubunge Zanzibar

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo, kimegoma kushiriki uchaguzi mdogo wa Ubunge Jimbo...

error: Content is protected !!