Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mahakama: Afande Rama hana hatia
Habari MchanganyikoTangulizi

Mahakama: Afande Rama hana hatia

Spread the love

Mahakama ya Mkoa wa Vuga mjini Unguja imemwachia huru mshtakiwa Ramadhan Ali maarufu kama Afande Rama aliyekuwa akikabiliwa na mashtaka ya kuingiliwa kinyume na maumbile. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Afande Rama ameachiwa huru leo Jumanne  baada ya hakimu wa mahakama hiyo, Khamis Simai kudai kuwa mshtakiwa hana hatia chini ya kifungu cha 220 ya sheria namba 7 ya mwaka 2018.

Kesi hiyo namba 59 ya mwaka 2023 ilianza kusikilizwa mahakamani hapo ambapo jumla ya mashahidi tisa kutoka upande wa mwendesha mashtaka waliwasilisha ushahidi wao ambao hawakuweza kumtia hatiani mtuhumiwa.

Ramadhani alishtakiwa baada ya kusambaa kwa video katika mitandao ya kijamii zilizodhaniwa kuwa ni yeye ambaye alionekana akishiriki tendo la kuingiliwa kinyume na maumbile.

Upande wa mashtaka ulikuwa unawakilishwa na muendesha mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar Mohd Saleh.

Afande Rama ambaye alikuwa Askari wa kikosi cha kutuliza gasia, kabla ya kushtakiwa, alivuliwa cheo cha uaskari na kubaki raia wa kawaida.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari Mchanganyiko

Wananchi washauriwa kuongeza uelewa wa kujikinga na majanga

Spread the love WITO umetolewa kwa wananchi kuongeza uelewa na utayari kabla...

error: Content is protected !!