Saturday , 18 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Kijana ahukumiwa jela maisha kwa kubaka mwanafunzi
Habari Mchanganyiko

Kijana ahukumiwa jela maisha kwa kubaka mwanafunzi

Mahakama
Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Shinyanga imemuhukumu kifungo cha maisha jela Hamza Butondo (32) baada ya kukutwa na hatia ya kumbaka mwanafunzi wa miaka 13.

Pia inadaiwa alimtishia kumchoma kisu mwanafunzi huyo iwapo angetoboa siri kwa unyama aliomtendea. Anaripoti Paul Kayanda …(endelea).

Akisoma hukumu hiyo mbele ya Mahakama hiyo, Hakimu mkazi Yusuph Zahoro alidai kuwa mahakama imemhukumu adhabu hiyo mtuhumiwa huyo baada kulidhibitika pasi na shaka kutokana na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo.

Alidai kuwa mahakama kwa kuzingatia sheria na ushahidi uliotolewa, mazingira ya utendaji wa kosa lenyewe amejiridhisha pasipo na shaka kwamba mshtakiwa anastahili adhabu hiyo.

Hakimu huyo alidai kuwa mshtakiwa huyo tarehe 11 Disemba 2022 maeneo ya Mhunze wilayani Kishapu mkoa wa Shinyanga muda wa saa 10 usiku.

Amedai alitenda kosa hilo kwa binti wa miaka 13 na kumtoa ndani na kumpeleka nje ya nyumba kwenye mto na kumfanyia unyama huo huku akimtishia kumchoma kisu iwapo atatoa siri.

Hata hivyo, Wakili wa Jamhuri, Jukaeli Jairo aliiomba mahakama hiyo itoe adhabu kali kwa kwa mshtakiwa huyo sababu mazingira ya kosa.

Pia wakili huyo alidai kuwa mshitakiwa katika maeneo anayoishi ni tishio katika jamii na pia ni mshtakiwa mwenye matendo ya kutisha na anakabiliwa na mashtaka mawili ambayo yako mahakamani hayajatolewa uamuzi.

Katika utetezi wake mshtakiwa Hamza Butondo aliiomba mahakama isimpe adhabu kali kwani anao watoto pia wazazi wake wanamtegemea na kwamba hawana wa kuwasaidia

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua bima ya afya kwa wakulima

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na kampuni...

Habari Mchanganyiko

Makamba awasili China kwa ziara ya kikazi

Spread the loveWaziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,...

Habari Mchanganyiko

Ethiopia yafungua njia ujenzi wa ubalozi Dodoma

Spread the loveSerikali ya Tanzania imeipongeza Serikali ya Ethiopia kwa kuweka historia...

error: Content is protected !!