Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mgodi wa Baraka wanufaisha wanakijiji
Habari Mchanganyiko

Mgodi wa Baraka wanufaisha wanakijiji

Spread the love

IMEELEZWA kuwa mgodi wa EBR and Partners maarufu Baraka uliopo katika kijiji cha Lyulu – Halmashauri ya wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita tangu uanze shughuli za uchimbaji wa madini ya dhahabu kwenye kijiji hicho umekuwa na manufaa makubwa kwa wananchi wa eneo hilo. Anaripoti Paul Kayanda, Shinyanga… (endelea).

Hayo yameelezwa jana tarehe 29 Januari 2023 na Meneja wa mgodi huo Sunday Tumaini alipozungumza na waandishi wa habari waliotembelea mgodi huo.

Meneja wa Mgodi wa EBR and Partners, Sunday Tumaini akifafanua jambo juu ya uwekezaji wa mgodi wake unaoendelea katika kijiji cha Lyulu kwa waandishi wa habari hawapo pichani.

Amesema kabla ya kuanza shughuli za uchimbaji wa madini katika eneo hilo kulikuwa na wananchi waliokuwa wanafanya shughuli hizo na kwa kuliona hilo Mkurugenzi wa Mgodi huo akawakatia kipande cha eneo kilichopo ndani ya leseni yake ili nao waendelee na shughuli ndogondogo za uchimbaji kwa ajili ya kujipatia kipato kuliko kuwatimua.

“Mgodi huu umekuwa na tija sana hususani kutokana na uzalishaji wake kwani wananchi wamepata ajira lakini pia Serikali imefaidika na kile kinachotoka hapa,” amesema Tumaini.

Aidha, amesema changamoto kubwa wanayokabiliana nayo ni miundombinu ya barabara na umeme hivyo anaiomba Serikali kuwasaidia kuboresha miundombinu ya barabara na pamoja na umeme ili kufikisha madini yanayochimbwa sokoni.

Ameongeza kuwa umeme utaongeza uzalisha kwa tija na serikali kuendelee kunufaika kutokana na uwekezaji wao kwa kutoa mirahaba na hata wananchi wanaozunguka eneo la mgodi nao wanufaike kupitia mgodi huo.

Katika hatua nyingine wamemshukuru Afisa Madini mkazi (RMO) wa Mbogwe kwa ushirikiano anaowapatia ukiwemo ushauri ambao kimsingi unawasaidia kwenye shughuli zao.

Akizungumzia faida za uwepo wa mgodi huo Tumaini amesema wamesaidia kutengeneza barabara kwa kiwango cha changarawe kutoka wilayani mpaka katika kijiji hicho ambako kuna uwekezaji wa mgodi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!