Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Shehena ya sigara bandia za Bil. 1.8/- kutoka DRC yakamatwa Shinyanga
Habari Mchanganyiko

Shehena ya sigara bandia za Bil. 1.8/- kutoka DRC yakamatwa Shinyanga

Spread the love

MAMLAKA ya Dawa na Vifaa tiba (TMDA), Kanda ya Ziwa Magharibi imekamata shehena ya sigara bandia zenye thamani ya Sh 1.8 Bilioni katika mkoa wa Shinyanga zikitokea nchini Congo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Shinyanga … (endelea)

Kwa mujibu wa taarifa kutoka TMDA, ofisi ya Kanda ya ZiwaMagharibi ilipokea taarifa ya kontena lenye bidhaa za tumbaku lililozuiliwa katika ofisi ya TRA Shinyanga na baada ya kwenda kuzikagua ikabainika kuwa sigara hizo ni bandia.

Taarifa hiyo iliyotolea leo Jumatano tarehe 28 Septemba, 2022 imeeleza kuwa shehena hiyo ilikuwa na jumla ya makasha 2200 yenye uzito tani 13.2.

“Makasha hayo yana uzito wa tani 13.2 kazi hii tulishirikiana kwa karibu sana na MCIE, lakini cha kujiuliza zimepitaje mipakani na tunao wakaguzi huko? Hatua zaidi zinaendelea kuchukuliwa na mzigo huu umezuiliwa,” amesema Gaudensia Simwanza Meneja wa Kitengo cha Uhusiano TMDA.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari Mchanganyiko

Wananchi washauriwa kuongeza uelewa wa kujikinga na majanga

Spread the love WITO umetolewa kwa wananchi kuongeza uelewa na utayari kabla...

error: Content is protected !!