Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Samia ahesabiwa, “maswali sio magumu”
Habari Mchanganyiko

Samia ahesabiwa, “maswali sio magumu”

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan amekuwa miongoni mwa Watanzania waliohesabiwa katika zoezi la Sensa ya Watu na Makazi iliyoanza saa 6:01 usiku wa leo Jumanne tarehe 23 Agosti, 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Rais Samia amehesabiwa mapema leo katika ikulu ya Chamwino jijini Dodoma na karani wa sensa ambaye awali alikuwa ameambatana na Mkurugenzi Mkuu wa ofisi ya Takwimu Tanzania (NBS), Albina Chuwa na Kamishna wa Sensa ya Watu na Makazi mwaka 2022, Anne Makinda.

Aidha, baada ya kumaliza kumhesabu, kazi iliyodumu si zaidi ya dakia 25, Rais Samia amesema, “nimemaliza kuhesabiwa, ni kweli maswali ni mengi kidogo lakini yanajibika, hakuna swali gumu.. ombi langu kwa wananchi ni kuweka taarifa zetu mapema.”

“Watu wa Takwimu, makamisaa walitoa maswali mapema, wananchi watafute hayo maswali ili waanze kutafutia majibu mapema.

“Mfano atauliza kama una bima ya afya, kadi ya NIDA namba ngapi, ukikaa nazo mkononi wanakwenda haraka. Kaya zetu wastani ni watu watano, kama hamkuwa tayari inaweza kuchukua muda mrefu,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

error: Content is protected !!