Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Dk. Yonazi asisitiza ushirikiano sekta binafsi, umma
Habari Mchanganyiko

Dk. Yonazi asisitiza ushirikiano sekta binafsi, umma

Spread the love

WATENDAJI wa taasisi za umma na binafsi ambao wanatekeleza ajenda ya kuipeleka nchi katika uchumi wa kidijiti wametakiwa kushirikiana na kutekeleza jukumu hilo kwa weledi na ubora wa viwango vya kimataifa. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea).

Akizungumza katika Jukwaa la Nne la Ubunifu na Teknolojia lililofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 19 Agosti, 2022, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dk. Jim Yonazi amesititiza ushirikishaji baina ya sekta ya umma na binafsi ili kutimiza malengo ya kuwa na Tanzania ya Kidijiti tunayoihitaji kwa maendeleo ya Taifa.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dk. Jim Yonazi (Kulia) akifatilia majadiliano ya Jukwaa la Nne la Ubunifu na Teknolojia yaliyokuwa na Kauli Mbiu ya Tanzania ya Kidijitali Tunayoihitaji, Hatua Zipi Zichukuliwe Kuifikia? lililoandaliwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) na kufanyika tarehe 19 Agosti, 2022 jijini Dar es Salaam.

Amesema kuwa, kuna fursa nyingi za kiuchumi katika ulimwengu wa kidijiti na Wizara hiyo ipo tayari kupokea na kufanyia kazi maoni ya wadau wa sekta ya umma na binafsi kuhusu nini kinahitaji maboresho katika kufikia dira na malengo ya Taifa ya kuijenga Tanzania ya Kidijiti.

Dk. Yonazi amezungumzia juhudi kubwa inayofanywa na Serikali ya kuongeza matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) inayoendesha uchumi wa kidijiti kwa kuongeza wigo wa usambazaji wa miundombinu na ufikishaji wa huduma za TEHAMA nchini.

“Kama mnavyofahamu hivi karibuni kupitia Shirika letu la Mawasiliano la TTCL tumefikisha intaneti yenye kasi katika Mlima Kilimanjaro na mradi wa kufikisha intaneti majumbani “fiber to home” tayari umeanza kutekelezwa na TTCL lengo ni kufikia uchumi wa kisasa wa kidijiti katika nchi yetu”, amesema Dk. Yonazi

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia Tanzania (COSTECH), Dk. Amos Nungu amesema kuwa Jukwaa la Ubunifu na Teknolojia limewakutanisha wataalamu wabobezi, watafiti, wabunifu na watunga sera ili kujadili na kutoka na taswira tofauti ya kuijenga Tanzania ya Kidijiti kwa kuangazia vipaumbele  na mahitaji ya watanzania.

Jukwaa hilo la Nne la Ubunifu na Teknolojia lilikuwa na kauli mbiu ya Tanzania ya Kidijitali Tunayoihitaji, Hatua zipi zichukuliwe Kuifikia? liliandaliwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP) kupitia programu ya ubunifu ya FUNGUO na kuwakutanisha wadau wa Sekta ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kutoka taasisi za umma na binafsi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

error: Content is protected !!