Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Majaliwa amgomea Sheikh kuoa mke wa pili
Habari Mchanganyiko

Majaliwa amgomea Sheikh kuoa mke wa pili

Spread the love

 

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amemueleza Sheikh Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum kwamba dua aliyomuombea ili aoe mke wa pili ni dua isyokubalika. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Majaliwa ametoa kauli hiyo leo tarehe 2 Julai, 2022 wakati akihutubia kilele cha Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Kupiga Vita Dawa za Kulevya duniani yanayofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

“Sheikh Alhad aliomba dua isiyokubali, nataka nimwambie wazee muda huu kule Peramiho wapo kanisani kupinga dua yako isikubalike,” amesema Majaliwa na kufanya umati uliohudhuria maadhimisho hayo kuangua kicheko.

Katika ufunguzi wa maadhimisho hayo, Sheikh Alhad amemuombea Waziri Mkuu aoe mke wa pili ilia pate utulivu zaidi katika mizunguko yake.

Katika dua hiyo ya ufunguzi Sheikh Alhad ameswali hivi; “Tunamuombea sana Waziri mkuu ambaye ndiye mgeni rasmi wa jambo hili, tumeshuhudia hasa sisi viongozi wa dini namna ambavyo na akijituma kwa ajili ya watanzania.

“Suala la sana suala la Ngorongoro, Loliondo… Waziri mkuu ammewathibitishia Watanzania kwamba serikali ina nia njema na raia wake na hakuna raia ambaye atakosa haki au kunyanyaswa kwa namna yoyote ile, amekuwa halali hapumziki.

“Tunamuombea Mwenyezi Mungu aendelee kumbariki Majaliwa Kassim Majaliwa na ikikupendeza aongeze pia mke wa pili aweze kupata utulivu zaidi katika mizunguko yake,” Sheikh Alhad Mussa Salum.

Waziri ameoa mke mmoja pekee anayefahamika kwa jina la Marry Majaliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy atangaza Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba

Spread the loveSERIKALI imesema imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha matibabu ya...

Habari Mchanganyiko

Shahidi aeleza namna Nathwani alivyomjeruhi jirani yake

Spread the loveMSIMAMIZI wa Msikiti wa Wahindi Lohana aitwae, Ankit Dawda (32)...

error: Content is protected !!