Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Majaliwa amgomea Sheikh kuoa mke wa pili
Habari Mchanganyiko

Majaliwa amgomea Sheikh kuoa mke wa pili

Spread the love

 

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amemueleza Sheikh Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum kwamba dua aliyomuombea ili aoe mke wa pili ni dua isyokubalika. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Majaliwa ametoa kauli hiyo leo tarehe 2 Julai, 2022 wakati akihutubia kilele cha Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Kupiga Vita Dawa za Kulevya duniani yanayofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

“Sheikh Alhad aliomba dua isiyokubali, nataka nimwambie wazee muda huu kule Peramiho wapo kanisani kupinga dua yako isikubalike,” amesema Majaliwa na kufanya umati uliohudhuria maadhimisho hayo kuangua kicheko.

Katika ufunguzi wa maadhimisho hayo, Sheikh Alhad amemuombea Waziri Mkuu aoe mke wa pili ilia pate utulivu zaidi katika mizunguko yake.

Katika dua hiyo ya ufunguzi Sheikh Alhad ameswali hivi; “Tunamuombea sana Waziri mkuu ambaye ndiye mgeni rasmi wa jambo hili, tumeshuhudia hasa sisi viongozi wa dini namna ambavyo na akijituma kwa ajili ya watanzania.

“Suala la sana suala la Ngorongoro, Loliondo… Waziri mkuu ammewathibitishia Watanzania kwamba serikali ina nia njema na raia wake na hakuna raia ambaye atakosa haki au kunyanyaswa kwa namna yoyote ile, amekuwa halali hapumziki.

“Tunamuombea Mwenyezi Mungu aendelee kumbariki Majaliwa Kassim Majaliwa na ikikupendeza aongeze pia mke wa pili aweze kupata utulivu zaidi katika mizunguko yake,” Sheikh Alhad Mussa Salum.

Waziri ameoa mke mmoja pekee anayefahamika kwa jina la Marry Majaliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!